Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini Mhe. Hussein Mohammed Bashe amekua na mkutano wa wazi na wananchi uliojikita katika kuelezea mafanikio na changamoto za miaka miwili ya kipindi cha ubunge wake.

Aidha Malengo makubwa ya mkutano huo yalikuwa ni:
1. Kusikiliza na kutatua kero za wananchi kwa uwazi ili kuongeza nafasi ya ushiriki na ushirikishwaji wa wananchi katika mijadala ya maendeleo.

2. Kueleza juhudi za kuleta maendeleo zilizokwishafanywa na Ofisi ya Mbunge katika kipindi cha miaka miwili (2)

3. Kutambulisha miradi mikubwa ya Elimu, Afya na Maji inayoendelea ndani ya Jimbo la Nzega Mjini;
Elimu
- Ujenzi wa Shule ya kwanza ya wanawake
- Utoaji wa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi wote wanaofaulu Jimboni kupitia Bashe Scholarship Awards 
- Ugawaji wa Vifaa vya shule na madaftari 37,000 
- Ujenzi wa Shule ya Kwanza ya Kidato cha Tano na Sita 
- Ujenzi wa zaidi ya vyumba vya madarasa 32 ya Shule za Msingi  kwenye kata 10 jimboni


 Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini Mhe. Hussein Mohammed Bashe akiwahutubia wananchi jimboni kwake katika mkutano wa wazi na wananchi,Mh Bashe alijikita katika kuelezea mafanikio na changamoto za miaka miwili ya kipindi cha ubunge wake.

 Baadhi ya Wananchi wa Nzega wakimsikiliza Mbunge wao,Mh Bashe alipokuwa akiwahutubia katika mkutano wa wazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...