Tarehe 20 Mei, 2017 Ofisi ya Makamu wa Rais iliutaarifu umma kuhusu utaratibu wa kufanya shughuli zote zinazohusu ukusanyaji, usafirishaji, biashara na urejeleshaji wa taka hatarishi kama vile vyuma chakavu, "Oil" chafu, matairi yaliyotumika, taka za kieletroniki na za umeme na taka zitokanazo na kemikali. 

Ofisi iliwataka wale wote wanaofanya shughuli hizi hapa nchini kufuata sheria, kanuni na miongozo. Aidha, kuzingatia utekelezaji wa mikataba ya kimataifa ya mazingira ambayo Tanzania ni mwanachama ikiwa ni pamoja na kuwa na vibali vya biashara husika.

Ofisi inapenda kuukumbusha umma kuwa bado baadhi ya wanaokusanya, kusafirisha na kurejeleza taka hatarishi hawana vibali kama inavyohitajika. Kanuni za Taka Hatarishi za mwaka 2009, kanuni ya 39 hadi 46 zinatoa muongozo wa hatua ambazo zinatakiwa kufuatwa ili shughuli husika zifanyike.

Hivyo, Ofisi inawakumbusha tena wale wote wanaofanya shughuli za uuzaji na ununuzi wa taka hizi kuhakikisha wanafanya biashara na wale wenye vibali tu. Hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 na Kanuni za Taka Hatarishi za mwaka 2009. 

Aidha, Kanuni ya 47 (3) ya Kanuni za Taka Hatarishi za mwaka 2009 inatoa adhabu kwa mtu ambaye anashindwa kufuata maelekezo yaliyotolewa, ambapo baada ya kufikishwa mahakamani na kupatikana na hatia anaweza kutozwa faini isiyopungua shilingi laki tano (500,000.00) au kifungo kisichopungua mwaka mmoja jela au vyote kwa pamoja. 

Mhandisi Joseph Kizito Malongo

KATIBU MKUU
OFISI YA MAKAMU WA RAIS

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...