Umoja wa Mataifa kupitia Umoja wa Vijana (YUNA) umetoa tuzo kwa Taasisi na watu binafsi wenye mchango mkubwa katika maisha ya watu barani Afrika.Kupitia tuzo hizo zinazotambulika kama PAHA, kituo cha Televisheni cha Clouds kimetambuliwa kama kituo bora cha Runinga kwa mwaka 2017.
Hiyo ni kutokana na kurusha maudhui yanayomulika maisha ya watu na kutoa tumaini kwao kupitia vipindi na kampeni mbalimbali kama vile...
(#IshiNaMimi #Kipepeo #MalkiaWaNguvu #RudishaTabasamuMiaMoyo na nyinginezo).

Baada ya kupokea tuzo hiyo ya heshima Kampuni ya Clouds Media Group imeishukuru YUNA pamoja na umoja na umoja wa mataifa kutokana na Utambuzi huo.

Sambamba na hilo Clouds Tv imewashukuru Watanzania Kwa kuendelea Kuwaamini na Kuwachagua." Tunaahidi kuendelea kuwatumikia kwa moyo na nguvu zaidi kwani tulishakula kiapo cha kuwa Taasisi ya watu" sehemu ya taarifa hiyo ilieleza.
(#RedioYaWatu #ThePeoplesStation).
#TunakufunguliaDuniaKuwaUnachotaka

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...