Na Dotto Mwaibale, Igunga Tabora

MKUU wa Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, John Mwaipopo amehitimisha zoezi la ugawaji wa mbegu bora katika mikoa ya Kagera, Geita na Tabora kwa kuipongeza Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kuwapelekea mbegu bora za mihogo, mahindi na Viazi lishe wilayani humo kwa kushirikiana na Jukwaa la Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB)

Pongezi hizo alizitoa jana wakati akizungumza na wakulima wa Kijiji cha Igogo kilichopo Kata ya Nanga katika uzinduzi na kukabidhiwa mbegu hizo kwa ajili ya mashamba darasa kwa wakulima wa vijiji vinne vya Igogo, Mwanzugi, Sungwizi na Busomeke.

Alisema changamoto kubwa waliyokuwa nayo wakulima katika Halmshauri hiyo ni kukosekana kwa mbegu bora za mihogo na mahindi jambo liliofanya uzalishaji wa mazao kuwa mdogo.

Mwaipopo alisema kuletewa kwa mbegu hizo kutaongeza mori wa kilimo kwa wakulima wa wilaya hiyo na kuondokana na ukosefu wa chakula badala ya kutegemea zaidi zao moja la mpunga.

Alisema kazi kubwa ya serikali ni kuhakikisha inasimamia utekelezaji wa mradi huo kwa nguvu zote ili kazi kubwa iliyofanywa na watafiti kutoka Vituo vya Ukiliguru Mwanza, Maruku mkoani Tabora na Ilonga mkoani Morogoro isipotee bure.
 Wakulima wa Kijiji cha Igogo wanaunda Kikundi cha Imala Makoye katika Halmashauri ya Wilaya ya Igunga mkoani Tabora wakiwa wameshika mbegu ya mahindi ya Wema 2109 baada ya kukabidhiwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) na Jukwaa la Bioteknolojia kwa Maendeleo ya Kilimo (OFAB) katika uzinduzi wa shamba darasa uliofanyika jana wilayani huo. Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo alikuwa mkuu wa wilaya hiyo, John Mwaipopo.
 Kaimu Ofisa Kilimo wa wilaya hiyo, Athumani Mgunya akizungumza kabla ya uzinduzi huo.
 Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi wa COSTECH ambaye ni Ofisa Mwandamizi wa COSTECH, Audax Mutagwa, akizungumza katika uzinduzi huo.
 Mkuu wa Wilaya ya Igunga, John Mwaipopo akizungumza na wakulima wa Kijiji cha Igogo wakati wa uzinduzi wa shamba darasa la mbegu ya mahindi. Kulia ni Ofisa Ugani wa Kata ya Nanga, Ambele Mwangomo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...