Viongozi wa vijiji, kata na
tarafa Wilayani Bukombe wametakiwa kutumia michango inayotolewa na wananchi kwa
shughuli zilizokusudiwa ili kuwaletea wananchi maendeleo katika maeneo yao.
Akizungumza katika kijiji cha
Kazibizyo kata ya Ng'anzo Wilaya ya Bukombe Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa
Mkoa wa Geita amesema katika vijiji,
kata na tarafa wananchi wamekuwa wakihimizwa kujitolea kuchanga michango ya
hiari ili kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo lakini baada ya michango
hiyo kukusanywa inatumika kwa maslahi binafsi ya Viongozi.
Amesema kuwa Viongozi hao wasio
na maadili wanapanga matumzi ya fedha za
wananchi bila kujali vipaumbele vya vijiji kwa maslahi yao binafsi vitendo
hivyo vinawavunja moyo wananchi wa kutoendelea kutoa michango ya maendeleo. "Kuna
vidudu vinavyoleta magonjwa watu wanasubili maendeleo hayatokei inabidi tuvitoe
tuvipige sindano kubwa vife humu humu viongozi wa namna hiyo wasio na maadili
wamekuwa wakihamishwa wakati hawajatoa taarifa za mapato na matumizi alah! kama
yupo Geita arudi arejeshe fedha za wananchi popote alipo".
Amesema kama kuna mtu au mtendaji
anayeona hatoshi apishe akae pembeni ili wanaoweza kufanya kazi wafanye ili
kuleta maendeleo ya haraka kwa wananchi. Hata hivyo, ametoa wito kwa wananchi
kutumia rasilimali zinazowazunguka kujiletea maendeleo badala ya kukaa na
kulalamika maisha magumu wakati kuna rasilimali nyingi katika maeneo
wanayoishi. Aidha, amezitaka Halmashauri
Mkoani Geita kusajili na kuvitumia vikundi vya mafundi vinavyojitolea kujenga
madarasa na Zahanati bila malipo katika miradi ya fedha katika maeneo
mbalimbali ili vijana hao wanufaike badala ya kutoa kazi zote kwa wakandarasi.
Awali Josephat Maganga Mkuu wa Wilaya ya Bukombe
amemweleza Mkuu wa Mkoa kuwa Wilaya ya Bukombe ina vijiji 52 na Vitongoji 372
lakini kuna Zahanati sita (6) tu za Serikali.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel akiwa Wilayani humo
amezindua kampeni ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na Zahanati katika vijiji
vya Kazibizyo na Bulama kwa kushiriki katika ujenzi na harambee iliyoleta
michango ya mifuko 93 ya simenti, fedha tasilimu shilingi 340000/=, tofali 500,mbao 50 na
misumari kilo3.
Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita (Aliyevaa kofia usalama) akishiriki kubeba mawe na wananchi kwa ajili ya ujenzi wa msingi katika Zahanati ya kijiji cha Kazibizyo Wilayani Bukombe.Wananchi wa kijiji hicho wanatembea umbali wa Kilometa 20 kwenda Ushirombo kupata huduma za afya.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel akishirikiana na mafundi wa ujenzi kujenga msingi wa Zahanati ya kijiji cha Kazibizyo alipotembelea kijiji hicho kuzindua kampeni ya ujenzi wa Zahanati na Vyumba vya madarasa.
Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kazibizyo Wilaya ya Bukombe baada ya uzinduzi wa kampeni ya ujenzi wa Madarasa na Zahanati Wilayi Bukombe.
Mhandisi Robert Gabriel akishirikiana na wananchi pamoja na viongozi wengine wa Wilaya ya Bukombe kuchanganya mchanga na sementi kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi kijiji cha Bulama.
Josephat Maganga Mkuu wa Wilaya ya Bukombe akizungumza na wananchi wa kijiji cha Bulama wakazi wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Geita kijijini hapo ili kuzindua kampeni ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na Zahanati. Habari na picha: Magesa
Jumapili - Afisa Habari Ofisi ya
Mkuu wa Mkoa Geita
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...