SHIRIKA lisilo la Kiserikali la Coconut Foundtion lenye Makao yake Makuu Kijitonyama Manispaa ya Kinondoni jijini Dar-es-Salaam, leo hii limewatangaza washindi kumi baada ya kumalizika kwa shindano la kutaja herufi sahihi ya sentensi za kiingereza, lililoanza Novemba 11.

Wahusika wa shindano hilo, walikuwa wanafunzi wa Shule za Msingi na Sekondari (English Medium School). Shindano hilo lilikuwa na lengo la kuwajengea uwezo na kujiamini katika matumizi ya lugha ya Kiingereza.

Washindi hao wanatarajia kwenda kwenye mashindano hayo nchini Uganda mnamo mwezi Desemba mwaka huu, ambako mashindano hayo yatazijumuisha nchi za Afrika Mashariki.

Shirika la Posta Tanzania lilikuwa miongoni mwa wafadhili wa shindano hilo.
Afisa Masoko Mwandamizi wa Shirika la Posta Tanzania, Bw. Philip Kowero akimkabidhi cheti Mwalimu wa kutoka Shule ya Feza baada ya shule yao, kufanya vizuri katika shindano hilo. 
Afisa Masoko Mwandamizi wa Shirika la Posta Tanzania, Bw. Philip Kowero akimkabidhi cheti mmoja wa wanafunzi baada ya shule yake, kuwa moja ya shule zilizoshiriki na kufanya vizuri katika shindano hilo.  
Washindi wakiwa wamekaa na zawadi zao walizotunukiwa. 
Baadhi ya washindi wa shindano la Nationa Spelling Bee wakiwa katika picha ya pamoja wa katikati ni mshindi kutoka Shule ya Feza, Bw. Adnan Abdallah. Kulia kwake ni Prokrith Ghandi kutoka Shule ya Aga Khan na kushoto ni Bi. Jackline, jijini Dar-es-Salaam. 
Walimu kutoka Shule mbalimbali na wazazi wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washindi wa shindano la National Spelling Bee, lililofanyika katika ukumbi wa jumba la Makumbusho jijini Dar-es-Salaam. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...