WIZARA ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, imeridhishwa na
ujenzi wa mradi wa jengo la tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege
cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBIII), ambapo
unatarajiwa kukamilika Septemba 2018. Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na
Mawasiliano (sekta ya Ujenzi), Mhe. Elias Kwandikwa wakati
alipotembea maendeleo ya mradi huo unaojengwa na Mampuni
ya ujenzi ya Bam International ya Uholanzi.
Mhe. Kwandikwa alisema mradi huo umefikia asilimia 66, ambapo
wizara imekuwa ikihakikisha mkandarasi analipwa kwa wakati ili
uweze kukamilika kama ilivyotarajiwa, na kukamilika kwake
kutatoa picha ya kuelekea kwenye Tanzania mpya.
“Hivi karibuni nilitembelea kiwanja cha KIA (Kiwanja cha Ndege
cha Kimataifa cha Kilimanjaro), nikaridhishwa na maendeleo ya
ukarabati unaoendelea pale, na nikaona ni vyema pia kutembelea
hili jengo na nimeliona na nimeridhishwa na kasi ya ujenzi
unaoendelea, ninaamini kama wakandarasi walivyosema basi
hadi kufikia Septemba 2018 litakuwa limekamilika kabisa,”
alisema Mhe. Kwandikwa.
Hata hivyo, Mhe Kwandikwa alisema serikali inajenga awamu ya
pili ya mradi huo kwa kutumia fedha za ndani, lakini pia kwa
kushirikiana na wadau wengine, ambapo ni ishara nzuri kuwa siku
zijazo kutakuwa na miradi mingi zaidi.
“Tunajenga mradi huu kwa fedha zetu za ndani, lakini pia kwa
kushirikiana na wadau wengine, hii ni ishara nzuri kwamba sasa
tunakokwenda tunao uwezo wa kuwa na miradi mingi zaidi kama
hii tuliojenga kwa kutumia fedha zetu wenyewe,” alisema Mhe.
Kwandikwa.
Hata hivyo, msimamizi wa Mradi huo, Mhandisi Barton Komba
alisema, mkandarasi wa ujenzi huo ameshalipwa fedha zake
zote, hivyo kwa sasa hadai serikali na anafanya kazi yake vizuri,
ili kukamilisha na kukabidhi jengo pindi litakapokamilika.
“Mpaka mwezi wa tisa mwakani utakuwa umekamilika kabisa,
lakini pia jengo hili limejengwa kwa kuzingatia viwango vya
kimataifa na litatoa huduma kwa watu wote hata ndugu zetu
wenye mahitaji maalumu, ,” alisema Mhandisi Komba.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhe. Elias
Kwandikwa (wa tatu kushoto) akielekea kwenye ukaguzi wa ujenzi wa jengo la abiria la Kiwanja
cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere. Wa pili kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Bw. Mtengela Hanga.
Msimamizi wa mradi wa ujenzi wa Jengo la Tatu la abiria la Kiwanja cha Ndege cha
Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBIII), Mhandisi Barton Komba (kulia) akimwonesha kitu
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhe. Elias Kwandikwa (wa
pili kulia), wakati alipotembelea na kukagua ujenzi wa jengo hilo.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Mhe. Elias
Kwandikwa (wa pili kulia), akizungumza na Mhandisi Barton Komba (wa tatu kushoto) wakati
wakitoka kwenye ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa mradi wa jengo la tatu la abiria la Kiwanja
cha ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...