Uongozi wa serikali ya awamu ya tano nchini Tanzania inayoongozwa na Dr. John Pombe Magufuli ni mfano wa kuigwa kwa nchi za Afrika kwa kuwa umekuwa makini kutumia vizuri rasilimali za nchi kwa manufaa ya watu wake.

Viongozi wengi wa kiafrika wamekuwa wakitumia vibaya rasilimali za nchi zao kwa kujilimbikizia mali huku wananchi wakibaki kuwa masikini wa kutupa. Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Dr. Magufuli unapambana na wanaofuja mali za uma pamoja na kuepuka sherehe na mikutano isiyo ya lazima ili kuokoa pesa kwa ajili ya kuendesha miradi ya maendeleo.

Hayo yalisemwa na Rev. Dr. Celestino Chishimba alipokuwa akiongoza sala maalumu ya kuadhimisha uhuru wa Tanzania iliyofanyika jumapili iliyopita kwenye kanisa la Anglican Holy Cross Cathedral jijini Gaborone nchini Botswana.

Ibada hiyo ilihudhuriwa na baadhi ya watanzania waishio nchini Botswana wakiongozwa na viongozi wa chama cha watanzania chini Botswana. Viongozi waliohudhuria ni Mwenyekiti, Bw. Nieman Kissasi, Makamu Mwenyekiti Bi Rehema Mselle Kalabamu, Katibu Bi Magret Tibesigwa na Mweka fedha Msaidizi Bi Haika Marandu. Historia fupi ya Tanzania ilitolewa na Eng. Ben Rugumyamheto.

Sherehe za kuadhimisha uhuru wa Tanzania zilihitimishwa na hafla iliyoandaliwa na Chama cha Watanzania nchini Botswana (ATB). Hafla hii ilifanyika kwenye kumbi za mikutano za Maharaja Gaborone juzi jumamosi. Mgeni rasmi kwenye hafla hii alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini anayehudumu pia Botswana, Mh. Silvester Ambokile.

Wageni wengine waliohudhuria sherehe hizi ni pamoja na Bw. Richard Lupembe kutoka ubalozi wa Tanzania uliopo Pretoria Afrika Kusini na mwenyekiti wa Chama cha Waganda nchini Botswana Bw. Jonathan Beesigomwe aliyeuwakilisha umoja wa wana Africa Mashariki nchini Botswana.

Mh. Balozi aliwapongeza wana jumuia ya watanzania nchini Botswana kwa kudumisha umoja na ushirikiano miongoni mwao kwani ni mfano wa kuigwa kusini mwa Afrika. Aliwasihi watanzania kukumbuka kuwekeza nyumbani Tanzania hasa wakati huu ambapo nchi yetu inahamasisha uwekezaji kwenye kilimo, elimu na viwanda.
Waumini waliohudhuria ibada maalumu ya kuiombea Tanzani wakimsikilisha Padre Chishimba alipokuwa akielezea kuhusu uongozi wa Tanzania wakati alipokuwa akihubiri.
Baadhi ya watanzania wakiimba wimbo wa Taifa wa Tanzania.
Padre Dr. Chishimba na Bw. Kissasi wakikata keki maalumu iliyoandaliwa ya kuadhimisha uhuru wa Tanzania. Wanaoshuhidia zoezi hilo ni Bi Rehema kalamabu na Eng. Ben Rugumyamheto
Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini anayehudumu pia Botswana, Mh. Silvester Ambokile akiwahutubia watanzania waliohuduria hafla ya kuadhimisha uhuru juzi jumamosi kwenye kumbi za Maharaja jijini Gaborone.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...