Mkazi wa Musoma, Robert Mwakatobe (37) amejishindia kitita cha sh milioni 6.5 kwa kubashiri kwa usahihi mchezo maarufu kwa ‘Perfect 12’ unaondeshwa na kampuni ya mchezo wa kubahatisha ya M-Bet.

Mwakatobe alikabidhiwa kitita chake jana na Afisa Habari wa Kampuni ya M-Bet, David Malley.

Malley alisema kuwa Mwakatobe alifanikiwa kubashiri sahihi jumla ya mechi 15 kati ya 17 na kuwa mshindi wao wa droo ya 17 tokea kuanzishwa kwa mchezo wa Perfect 12. Alisema kuwa serikali imejipatia jumla ya Sh milioni 11 kutoka kiasi hicho cha fedha ambacho ni asilimia 18 kwa mujibu wa sheria.

“Kama tulivyosema hapo awali, M-Bet ni nyumba ya washindi, tumedhihirisha usemi wetu ambapo Mwakatobe anajishindia mamilion ya fedha kwa kutumia kiasi cha She elfu moja tu, hii imedhihirisha kuwa tunawaomba mashabiki wa soka kuendelea kucheza mchezo wetu ili kujishindia fedha,” alisema Malley.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa fedha zake, Mwakatobe alisema kuwa atazitumia fedha hizo kwa kupanua biashara yake ya kuuza dagaa. “Nilikuwa nafanya biashara ya kuuza gunia mbili tu za dagaa, sasa natarajia kununua fuso na kuuza dagaa pamoja na biashara nyingine ambazo nitazifikiria hapo baadaye,” alisema Mwakatobe.

Aliwataka watanzania kutokata tamaa katika michezo ya kubashiriki kwani lazima waamini kuwa ipo siku watashinda na kubadili maisha kama yeye.
“Sitaacha kucheza, nitaendelea kufanya ili kuweza kupata fedha zaidi na kuwa katika miongoni mwa wafanyabiashara wakubwa hapa nchini, mtaji huu umenifanya kuwa mtu tofauti na si wa kuuza kwa visado au debe na mafungu,” alisema.

 Afisa Habari wa Kampuni ya M-Bet, David Malley (kushoto) akimkabidhi hundi mshindi wa mchezo wa Perfect 12, Robert Mwakatobe (kulia) ambaye amejishindia kitita cha sh milioni 61.5
 Mshindi wa mchezo wa Perfect 12 Robert Mwakatobe 'akipozi' na mfano wa hundi mara baada ya kukabiziwa jana. Mwakatobe  alijishindia kitita cha sh milioni 61.5
Afisa Habari wa Kampuni ya M-Bet, David Malley (kushoto) na Mshindi wa Perfect 12, Robert Mwakatobe wakishangilia mara baada ya kukabidhiana zawadi.  Mwakatobe alishindia kitita cha sh milioni 61.5 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...