Rais wa Palestina Mheshimiwa “Mahmuud Abbas” katika hotuba yake kwenye Mkutano wa dharura wa Kiislamu uliofanyika nchini Uturuki, kujadili azimio la Rais wa Marekani Donald Trump la kuitambua Jerusalem kuwa ni mji mkuu wa Israeli, amemshukuru Papa Francis, nchi zote na viongozi wa nchi hizo, waliotangaza kwa pamoja msimamo wao wa waziwazi na unaopinga matendo yasiyofaa ya Rais wa Marekani, huku wakisimama kidete na wananchi wao dhidi ya azimio hilo lisilo la kisheria.
Aidha, Rais Abbas ameweka wazi ya kwamba taifa la Palestina na mataifa yote kiarabu, wakiwemo waislamu na wakristo wanaungana katika kulikabili azimio hili lisilo sahihi na linalokwenda kinyume na maazimio yote ya Baraza la Usalama, Mahakama ya Kimataifa ya Haki na maazimio ya Mashirika yote ya kikanda na kimataifa, yanayoshughulikia mgogoro wa Palestina na Israeli yakiwemo maazimio ya Umoja wa Afrika.
Rais Mahmuud Abbas  wa Palestina  pia ametilia mkazo kuwa, hakuna amani itakayopatikana bila ya kutambulika Jerusalem ya mashariki kama ni mji mkuu wa dola ya Palestina na kwamba Wananchi wa Palestina wataendelea kusimama kidete katika ardhi yao na kulinda sehemu takatifu za kikristo na kiislamu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...