Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amesimamisha shughuli za uvuvi katika ziwa Rukwa hadi hapo wataalamu wa afya watakapojiridhisha kuwa hakuna ugonjwa wa kipindupindu katika kambi za uvuvi zinazozunguka ziwa hilo na Mkoa kwa jumla.

Amesema kuwa athari inayopatikana katika kambi hizo za uvuvi zitawaathiri wala samaki unaotokana na uvuvi wa ziwa hilowaliopo na kuongeza kuwa wale wote wanaovua samaki waliopiga kambi katikakati ya ziwa waache kuvua mara moja na wasiruhusiwe kuingia katika ili kuweza kuudhibiti ugonjwa huo.

“Kuanzia leo tunapiga marufuku shughuli zote za uvuvi, mpaka tutakapojiridhisha kwamba tuna mazingira safi na salama, na kwamba maisha yetu hayapo hatarini tena na hao mnaosema wanakuja hawatapata maeneo ya kuuzia samaki wao tena watatafuta pa kwenda na tutaweka kambi ya kudhibiti wagonjwa wanaotoka huko wataishia hapa hawatakwenda popote,” Alisisitiza.

Ameyasema hayo alipofanya ziara katika kambi ya mererani iliyopo katika kijiji cha Ilanga, Kata ya Muze Wilaya ya Sumbawanga katika bonde la Ziwa Rukwa ambapo mpaka anafiak hapo palikuwa na wagonjwa 9 wa kipindupindu..
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akizungumza na wananchi wa kijiji cha Ilanga, katika kambi ya wavuvi Mererani, Wilayani Sumbawanga (hawapo kwenye picha) mara baada ya kufanya ziara katika kambi hiyo ili kujionea mazingira ya kambbi hiyo na hali ya kipindupindu.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akizungumza na wananchi wa kijiji cha Ilanga, katika kambi ya wavuvi Mererani, Wilayani Sumbawanga , mara baada ya kufanya ziara katika kambi hiyo ili kujionea mazingira ya kambbi hiyo na hali ya kipindupindu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...