Na Mwandishi Wetu
SERIKALI kupitia Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Nchini (DCEA) imesema ipo mbioni kutoa mwongozo wa kuratibu na kusimamia viwango vinavyowiana vinavyotarajiwa kutumika katika Vituo  vyote vya Upataji nafuu kwa watumiaji wa dawa za kulevya nchini.
Hayo yamesemwa jana Jijini Dar es Salaam na Mratibu wa Mashirika yasiyo ya Serikali NGO’s kutoka (DCEA), Salome Mbonile wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka minne ya kituo cha upataji nafuu kwa watumiaji wa dawa za kulevya (PEDDEREF) kilichopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam.
Mbonile alisema katika kuhakikisha kuwa mwongozo huo unaleta tija iliyokusudiwa, Serikali inatarajia kuwashirikisha wadau wote katika mapambano dhidi ya madawa ya kulevya ili waweze kutoa mapendekezo, ushauri na maoni ili kuweza kuisaidia jamii hususani makundi ya vijana katika kujiepusha na matumizi ya madawa ya kulevya.
"Kumekuwa na uwoga kwa wananjamii kutembelea Sober House (Nyumba za upataji nafuu kwa watumiaji wa madawa ya kulevya, lakini kupitia mwongozo huu tunataka kuweza viwango vinavyofanana ili kutoa fursa kwa watu wote kutembelea makazi haya" alisema Mbonile.
Mbonile alisema mapambano ya vita dhidi ya matumizi ya madawa ya kulevya nchini hayana budi kuungwa mkono na wadau mbalimbali wa maendeleo na hivyo Serikali itaendelea kutoa ushirikiano wa na asasi, taasisi mbalimbali ili kuhakikisha kuwa jamii ya Kitanzania hususani vijana inaendelea kuwa salama na kuondokana na matumizi ya dawa za kuelvya.
Aliongeza kuwa hadi sasa Tanzania ina jumla ya Nyumba za upataji nafuu kwa watumiaji wa dawa za kulevya 25 pamoja na Asasi 16 zinazotoa elimu na kuhamasisha jamii kutambua madhara mbalimbali yatokanayo na matumizi ya dawa za kulevya ikiwemo hatari ya maambuzi ya magonjwa mbalimbali pamoja na vifo.
 Mratibu wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGO's) kutoka Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Bibi. Salome Mbonile akizungumza wakati wa hafla ya kusherehekea miaka minne tangu kuanzishwa kwa Kituo cha Upataji nafuu kwa watumiaji wa Dawa za Kulevya (PEDDEREF) kilichopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni Msimamizi wa Programu wa Kituo hicho Khamis Ajib Dimand  na Mkurugenzi na Mwanzilishi wa kituo hicho Bi. Nuru Salehe Ahmed.
 Mkurugenzi na Mwanzilishi wa kituo hicho Bi. Nuru Salehe Ahmed akizungumza wakati wa hafla ya kusherehekea miaka minne tangu kuanzishwa kwa Kituo cha Upataji nafuu kwa watumiaji wa Dawa za Kulevya (PEDDEREF) kilichopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam jana. Kutoka kushoto ni Msimamizi wa Programu wa Kituo hicho Khamis Ajib Dimand  na Mratibu wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali(NGO's) kutoka   Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Bibi. Salome Mbonile (katikati).
 Mmoja wa wanufaika wa Kituo cha upataji nafuu kwa watumiaji wa dawa za kulevya (PEDDEREF) kilichopo Kigamboni Jijini Dar es Salaam Bi. Amina Mbonde akitoa ushuhuda namna alivyofanikiwa kuacha matumizi ya dawa za kulevya  wakati wa hafla ya kusherehekea miaka minne tangu kuanzishwa kwa kituo hicho jana. Kutoka kulia ni Mkurugenzi na Mwanzilishi wa kituo hicho Bi. Nuru Salehe Ahmed, Msimamizi wa Programu wa Kituo hicho Khamis Ajib Dimand  na Mratibu wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGO's) kutoka   Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Bibi. Salome Mbonile na Msimamizi wa Programu wa Kituo hicho Khamis Ajib Dimand.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...