Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Edmund Benard Mndolwa akitangaza kutengua ushindi wa Nuru Kassim Bainaga aliyetangazwa kuwa mjumbe wa Baraza Kuu la Jumuiya ya  Wazazi kwenda kwenye Umoja wa Wanawake (UWT) na kumtangaza Zainabu Zubeir Sige kuwa mshindi halali wa nafasi hiyo Picha na Mpiga picha Wetu.

TAARIFA KUTOKA JUMUIA YA WAZAZI YA CCM.

Uongozi wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) chini ya Mwenyekiti wake Ndg. Dkt. Edmund Mndolwa, leo tarehe 16 Desemba 2017 umekamilisha kuhakiki matokeo ya kura zilizopigwa katika Jumuia hiyo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wajumbe wa Jumuia hiyo walioshiriki katika uchaguzi uliofanyika tarehe 13 Desemba 2017

Katika taarifa yake Ndg. Dkt. Mndolwa amesema matokeo yaliyotangazwa na kumpa ushindi Ndg. Nuru Kassian Bainaga kwa nafasi ya WAZAZI kwenda UWT, yanatenguliwa na badala yake, amemtangaza Ndg. Zainab Zuberi Sige kuwa mjumbe halali wa WAZAZI kwenda UWT.

Huu ni muendelezo wa kuhakikisha kuwa haki inatendekea katika chaguzi mbalimbali za Chama na Jumuia zake.

Imetolewa na,

IDARA YA ITIKADI NA UENEZI
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...