Kampuni ya Tanzania Mortgage Refinance Company Limited (TMRC), imetoa zawadi ya Sikukuu ya Krismas zenye thamani ya Shilingi Milioni Mbili (Shilingi 2,000,000) kwa Kituo cha Watoto yatima cha Kiwalani (Kiwalani Orphanage Centre) kilichopo jijini Dar es Salaam.
Zawadi hizo zimekabidhiwa leo na Afisa Mtendaji Mkuu wa TMRC, Bw. Oscar P. Mgaya kwa Mkurugenzi wa Kituo hicho, Mchungaji   Elias Mwakalukwa -, katika ghafla iliyofanyika kwenye Kituo hicho kilichopo jijini Dar es Salaam.
Miongoni mwa zawadi zilizotolewa kwa kituo hicho cha watoto yatima ni pamoja na mchele, mafuta ya kupikia, unga wa sembe, maharage, sabuni za kufulia na kuogea, sukari ,  chumvi,  dawa za meno, majani, kalamu na madaftari
“Kwa upendo wetu wa dhati kabisa tumeona umuhimu wa kushiriki pamoja na watoto yatima, ambao wapo katika mazingira magumu, katika kusherehekea Sikukuu ya Krimas mwaka 2017,” alisema Bw. Mgaya.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...