VIJANA nchini wametakiwa kutambua wajibu wao katika Taifa kwa kutumia fursa zinazojitokeza kuwania nafasi mbalimbali za Uongozi katika jamii ili kutetea maslahi na agenda mbalimbali zinazogusa maendeleo yao.

Hayo yamesemwa leo Jumamosi (Desemba 17, 2017) Jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Ushawisihi na Utetezi wa Taasisi ya Vijana ya TYVA, Yusuf Bwango wakati wa mdhahalo wa vijana uliolenga kuwajengea uwezo wa kutumia mitandao ya kijamii katika kutetea maslahi yao.

Kwa mujibu wa Bwango alisema tafii mbalimbali zimebaini kuwa Vijana wengi wamekuwa na mtazamo hasi kujitokeza kuwania nafasi mbalimbali za Uongozi hususani Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, na kubaki nyuma katika nafasi hizo huwaniwa na kushindaniwa na Wazee pekee.

“Tumefanya mdahalo huu kwa malengo ya kuwajengea uwezo vijana kutambua kuwa wao ndio Viongozi wa baadae na hili litaanzia katika chaguzi mbalimbali zinazofanyika katika ngazi za kijamii ikiwemo chaguzi za Serikali za Mitaa” alisema Bwango.

Bwango alisema umefika wakati kwa Vijana wa Kitanzania kuweza kutumia majukwaa mbalimbali ili kuweza kubadili fikra na mitazamo yao kuhusu mifumo ya kiutawala na kutumia majukwaa hayo kuunda vyombo imara vitakavyoweza kuwasilisha na kupaza sauti zao.
1. Bi. Sumaiya Mahmoud kutoka Taasisi ya Mwanamke na Uongozi akichangia hoja wakati wa mdahalo wa vijana ulioandaliwa na Taasisi ya Vijana ya TYVA uliolenga kuwajengea uwezo wa kutumia mitandao ya kijamii katika kutetea maslahi yao. Mdahalo huo ulifanyika leo Jumamosi Desemba 16, 2017 katika hoteli ya Regency Park Jijini Dar es Salaam.
1. Baadhi ya Vijana kutoka sehemu mbalimbali za Jijini wakifuatilia mdahalo wa vijana ulioandaliwa na Taasisi ya Vijana ya TYVA uliolenga kuwajengea uwezo wa kutumia mitandao ya kijamii katika kutetea maslahi yao. Mdahalo huo ulifanyika leo Jumamosi Desemba 16, 2017 katika hoteli ya Regency Park Jijini Dar es Salaam.
1. Bw. Oscar Munga akichangia hoja wakati wa mdahalo wa vijana ulioandaliwa na Taasisi ya Vijana ya TYVA uliolenga kuwajengea uwezo wa kutumia mitandao ya kijamii katika kutetea maslahi yao. Mdahalo huo ulifanyika leo Jumamosi Desemba 16, 2017 katika hoteli ya Regency Park Jijini Dar es Salaam.
1. Bi. Anna Winstone akichangia hoja wakati wa mdahalo wa vijana ulioandaliwa na Taasisi ya Vijana ya TYVA uliolenga kuwajengea uwezo wa kutumia mitandao ya kijamii katika kutetea maslahi yao. Mdahalo huo ulifanyika leo Jumamosi Desemba 16, 2017 katika hoteli ya Regency Park Jijini Dar es Salaam.
1. Mmoja wa washiriki wa mdahalo wa vijana ulioandaliwa na Taasisi ya Vijana ya TYVA uliolenga kuwajengea uwezo wa kutumia mitandao ya kijamii katika kutetea maslahi yao. Mdahalo huo ulifanyika leo Jumamosi Desemba 16, 2017 katika hoteli ya Regency Park Jijini Dar es Salaam.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...