Serikali imeiagiza Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Shanta Mining Limited inayofanya shughuli zake Mkoani Singida kuharakisha ulipaji fidia kwa wananchi waliopisha maeneo yao ili shughuli za uchimbaji zianze mara moja.
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo alitoa agizo hilo Desemba 12, 2017 wakati wa ziara yake ya kutembelea migodi ya dhahabu katika wilaya za Ikungi na Manyoni ili kujionea shughuli zinazoendelea pamoja na kuzungumza na wachimbaji wa madini.
“Mchakato wa fidia ufanyike haraka na mgodi uanze shughuli zake za uchimbaji mapema,” aliagiza Naibu Waziri Nyongo.
Akiwa njiani kuelekea kwenye Mgodi wa Dhahabu wa Elizabeth Shango uliopo katika Kijiji cha Sambaru, msafara wake ulisimamishwa na wananchi katika Kijiji cha Mang'onyi, Kata ya Mang'onyi, wilayani Ikungi ambao walilalamika kuzuiwa kuendeleza maeneo yao na kampuni hiyo na huku wakicheleweshewa kulipwa fidia.
Walisema kuwa tayari wameachia maeneo waliyokuwa wakimiliki kwa kufanya shughuli mbalimbali zikiwemo kilimo na uchimbaji mdogo wa madini ya dhahabu ili kupisha shughuli za uchimbaji mkubwa lakini Kampuni hiyo ya Shanta bado haijakamilisha ulipaji wa fidia.
Naibu
Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati) akizungumza na wananchi
wa Kijiji cha Mang'onyi, Kata ya Mang'onyi, wilayani Ikungi
waliosimamisha msafara wake (hawapo pichani)
Baadhi
ya wananchi wa Kijiji cha Mang'onyi, Kata ya Mang'onyi, wilayani Ikungi
wakimsikiliza Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (hayupo
pichani).
Naibu
Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (mbele katikati) akiwa nyumbani kwa
Mzee Bastan Mtundwi (mbele kulia) na mkewe Esta Mtundwi ambao
walijengewa Nyumba na Kampuni ya Shanta ikiwa ni fidia ya kupisha eneo.
Baadhi
ya wananchi wa Kijiji cha Mang'onyi, Kata ya Mang'onyi, wilayani Ikungi
wakimsikiliza Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Kwahili sikubaliani na selikali. Kama eneo analomiliki mwananchi lina madini ya thamani $1billion fidia atakayopewa kwa eneo lake ni kiasi gani?
ReplyDelete