Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.

Kijana mzalendo, Omary Kombe amejipanga kutembea kutoka Kimara hadi Kivukoni siku ya Jumamosi, Januari 20, 2018 ili kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika kuliletea Taifa maendeleo.

Kombe ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya nia ya matembezi yake pamoja na mpango wake wa kutoa tuzo kwa Rais Magufuli itakayojulikana kama ‘Tuzo ya Kiongozi Mzalendo’.

Kombe amesema kuwa Rais Magufuli amekuwa ni kiongozi makini, mwenye uthubutu, mwenye msimamo thabiti na mzalendo wa kweli kwani amefanya mambo mbalimbali yakiwemo ya kuimarisha mfumo wa ulipaji kodi, kubadilisha sheri kandamizi za madini, kukomesha vitendo vya ujangili katika mbuga za wanyama, rushwa na dawa za kulevya pia kurejesha nidhamu kwa watumishi wa umma.

“Kubwa kuliko yote, Serikali ya Awamu wa Tano kwa ujumla imekuwa ikihamasisha kwa vitendo kuhusu ujenzi wa Tanzania ya Viwanda na kupelekea nchi kuwa na uchumi wa kati hivyo kwa niaba ya vijana wazalendo napenda kumpongeza kwa kufanya matembezi, kumpa tuzo ya kiongozi mzalendo pamoja na kutoa msaada katika hospitali ya Ocean Road iliyopo jijini hapa,” alieleza Kombe.
Kijana Mzarendo,Omary Kombe akizungumzana na waandishi wa hawapo pichani juu ya kutembea kutoka Kimara hadi Kivukoni siku ya Jumamosi, Januari 20,mwaka huu ili kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika kuliletea Taifa maendeleo, Mwenyekiti Mwenza Kamati ya Kutoa Elimu ya Unyonyaji kwa Watu Wenye Ualbino, Maiko Lugendo.
Mwenyekiti Mwenza Kamati ya Kutoa Elimu ya Unyonyaji kwa Watu Wenye Ualbino,Maiko Lugendo akimkabdhi Kijana Mzarendo,Omary Kombe t-shirt atakayo vaakesho kwaajili ya matembezi hayo.picha na Emmanuel Massaka,Globu ya jamii.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...