NA WAMJW-DAR ES SALAAM

ASILIMIA 80 ya wanaohitaji damu nchini ni wanawake kwa sababu mbalimbali ikiwemo uzazi salama wakati wa kujifungua kwa njia ya kawaida na njia ya upasuaji. 

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuchangia damu ambayo inafanywa na Chama cha wanawake wa Tasnia ya Filamu nchini leo jijini Dar es salaam. 

“Napenda kusisitiza Damu haiuzwi na kwa mgonjwa yeyote atakayeuziwa damu kwenye kituo chochote cha afya cha Serikali atoe taarifa kwenye idara husika na atachukuliwa hatua” alisisitiza Waziri Ummy Mwalimu. 

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa Uongozi wa Hospitali au kituo cha Afya cha Serikali wahakikishe kuwa wanaweka matangazo yanayoelimisha wananchi kuwa damu haiuzwi bali inatolewa bila ya malipo na matangazo yaelekeze wananchi sehemu ya kutoa malalamiko. 
Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu aliyesimama akiongea na wananchi hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuchangia damu iliyoandaliwa na Chama cha wanawake cha Tasania ya Filamu nchini leo jijini Dar es salaam.
Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu aliyesimama kushoto akimsalimia mwananchi anayepata huduma katika moja ya banda lililokuwa likitoa huduma za afya katika viwanja vya Biafra wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuchangia damu iliyoandaliwa na Chama cha wanawake cha Tasania ya Filamu nchini leo jijini Dar es salaam.
Waziri wa afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wasanii wa kike wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuchangia damu iliyoandaliwa na Chama cha wanawake cha Tasania ya Filamu nchini leo jijini Dar es salaam.
Baadhi ya wasanii wakiwa wanasubiri huduma ya kuchangia damu wakati wa uzinduzi wa kampeni ya kuchangia damu iliyoandaliwa na Chama cha wanawake cha Tasania ya Filamu nchini leo jijini Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...