Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga amewahakikishia wamiliki wa viwanda vya mazao ya misitu   nchini kuwapa ushirikiano wa kutosha pale inapohitajika kwa kuzishughulikia  changamoto mbalimbali zinazowakabili  ili kwenda sambamba na azma ya serikali ya awamu ya tano  ya Tanzania ya viwanda.
Amesema   Wizara ya Maliasili na Utalii  imedhamiria   kutatua changamoto zinazowakabili  ili kuwawezesha  wamiliki wa viwanda hivyo hasa  wazawa  kutoa  ajira nyingi kwa wananchi.
Amesema  Wizara hiyo haiwezi kufanya kazi pekee yake pasipo  kushirikiana  na sekta binafsi kwani  wao ndo wamiliki wa viwanda vinavyotoa ajira kwa wananchi ambao ndio walinzi wakubwa   misitu nchini.
Akizungumza kwenye kikao kilichofanyika jana mjini Dodoma, kati ya  viongozi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) na  Wawakilishi wa Wamiliki wa Viwanda vya mazao ya misitu nchini,  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga aliwataka wadau hao  wasisite kuwasiliana nae pale wanapokuwa na jambo lolote linalohusu maendeleo ya viwanda vyao
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (katikati) akizungumza na  Rais wa Shirikisho la viwanda vya misitu Tanzania (SHIVIMITA) Ben Sulus  (kulia) wakati Rais  huyo  alipokuwa  akiwasilisha  taarifa  ya  wamiliki wa viwanda vya mazao ya misitu  wakati wa kikao   kilichofanyika jana  mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni muendelezo wa viongozi wa  Wizara kukutana na wadau wa Wizara  kuwasikiliza na kuzifanyia kazi changamoto zinazowakabili. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa  ( Picha na Lusungu Helela-MNRT) 
 Rais wa Shirikisho la viwanda vya misitu Tanzania (SHIVIMITA) Ben Sulus  akiwasilisha  taarifa  ya  wamiliki wa viwanda vya mazao ya misitu kwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga  wakati wa kikao   kilichofanyika jana  mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni muendelezo wa viongozi wa  Wizara kukutana na wadau wa Wizara kuwasikiliza na kuzifanyia kazi changamoto zinazowakabili. 
 Baadhi ya  wawakilishi wa wamiliki wa viwanda vya mazao ya misitu  wakimsikiliza  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii , Japhet Hasunga  kwenye  kikao    kilichofanyika jana  mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni muendelezo wa viongozi wa  Wizara kukutana na wadau wa Wizara  kuwasikiliza na kuzifanyia kazi changamoto zinazowakabili. 
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa akizungumza  kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga  kufungua  kikao cha  wawakilishi wa wamiliki wa viwanda vya mazao ya misitu  kilichofanyika jana  mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni muendelezo wa viongozi wa  Wizara kukutana na wadau wa Wizara  kuwasikiliza na kuzifanyia kazi changamoto zinazowakabili.  
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wawakilishi wa wamiliki wa viwanda vya mazao ya misitu  mara baada   kufungua kikao    kilichofanyika jana  mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni muendelezo wa viongozi wa  Wizara kukutana na wadau wa Wizara  kuwasikiliza na kuzifanyia kazi changamoto zinazowakabili. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...