Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga amewahakikishia wamiliki wa
viwanda vya mazao ya misitu nchini kuwapa ushirikiano wa kutosha pale
inapohitajika kwa kuzishughulikia
changamoto mbalimbali zinazowakabili ili kwenda sambamba na azma ya serikali ya
awamu ya tano ya Tanzania ya viwanda.
Amesema Wizara ya Maliasili na Utalii imedhamiria kutatua
changamoto zinazowakabili ili
kuwawezesha wamiliki wa viwanda hivyo
hasa wazawa kutoa ajira nyingi kwa wananchi.
Amesema
Wizara hiyo haiwezi kufanya kazi pekee
yake pasipo kushirikiana na sekta binafsi kwani wao ndo wamiliki wa viwanda vinavyotoa ajira
kwa wananchi ambao ndio walinzi wakubwa misitu nchini.
Akizungumza
kwenye kikao kilichofanyika jana mjini Dodoma, kati ya viongozi wa Wakala wa Huduma za Misitu
Tanzania (TFS) na Wawakilishi wa
Wamiliki wa Viwanda vya mazao ya misitu nchini,
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga aliwataka wadau hao wasisite kuwasiliana nae pale wanapokuwa na
jambo lolote linalohusu maendeleo ya viwanda vyao
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (katikati) akizungumza na Rais wa Shirikisho la viwanda vya misitu Tanzania (SHIVIMITA) Ben Sulus (kulia) wakati Rais huyo alipokuwa akiwasilisha taarifa ya wamiliki wa viwanda vya mazao ya misitu wakati wa kikao kilichofanyika jana mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni muendelezo wa viongozi wa Wizara kukutana na wadau wa Wizara kuwasikiliza na kuzifanyia kazi changamoto zinazowakabili. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa ( Picha na Lusungu Helela-MNRT)
Rais wa Shirikisho la viwanda vya misitu Tanzania (SHIVIMITA) Ben Sulus akiwasilisha taarifa ya wamiliki wa viwanda vya mazao ya misitu kwa Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga wakati wa kikao kilichofanyika jana mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni muendelezo wa viongozi wa Wizara kukutana na wadau wa Wizara kuwasikiliza na kuzifanyia kazi changamoto zinazowakabili.
Baadhi ya wawakilishi wa wamiliki wa viwanda vya mazao ya misitu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii , Japhet Hasunga kwenye kikao kilichofanyika jana mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni muendelezo wa viongozi wa Wizara kukutana na wadau wa Wizara kuwasikiliza na kuzifanyia kazi changamoto zinazowakabili.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa akizungumza kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga kufungua kikao cha wawakilishi wa wamiliki wa viwanda vya mazao ya misitu kilichofanyika jana mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni muendelezo wa viongozi wa Wizara kukutana na wadau wa Wizara kuwasikiliza na kuzifanyia kazi changamoto zinazowakabili.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wawakilishi wa wamiliki wa viwanda vya mazao ya misitu mara baada kufungua kikao kilichofanyika jana mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni muendelezo wa viongozi wa Wizara kukutana na wadau wa Wizara kuwasikiliza na kuzifanyia kazi changamoto zinazowakabili. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Dkt. Ezekiel Mwakalukwa.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...