Kitengo cha Mawasiliano WAMJW

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) amezidua Saccoss ya Wanawake katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya kwa ajili ya wajasiriamali wadogowadogo ili kuweza kutatua changamoto zao na kuwawezesha kupa mbinu mbalimbali za kufanikisha matarajio yao na kupata maendeleo.

Ameizindua Saccoss hiyo Mkoani Mbeya wakati akiitambulisha Programu ya ‘Kikundi Mlezi’ katika Manispaa ya ya Jiji la Mbeya yenye lengo la kuwawezesha wanawake wajasirimali kuwezeshana kati yao wenyewe katika kuanzisha na kuendeleza miradi ya biashara.

Dkt. Ndugulile amesema kuwa katika zoezi la kuamsha ari ya wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo linaenda sambamba na uwezeshwaji wa wanawake katika kuwashirikisha wanawake wenyewe katika kuibua miradi na kuanzisha shughuli za uzalishaji kwa kuzingatia matumizi ya fursa na weledi wa wananchi wenyewe. 

Dkt.Ndugulile amesema kuwa ili kufanikisha kufikiwa kwa Tanzania ya viwanda Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wajasiriamali wadogo wadogo hasa wanawake kuwaweza kuanzisha vikundi vitakavyoanzisha viwanda vidogo vidogo na kuzalisha bidhaa zitakazo uzwa ndani na nje ya mkoa wa Mbeya na hivyo kuutangaza mkoa kupitia bidhaa zilizozalishwa kwa kutumia ubunifu na rasilimali zilizopo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) akiangalia bidhaa ya Tea Masala wakati alipotembelea moja ya Kikundi cha wanawake wajasiriamali cha kilichopo Manispaa ya Jiji la Mbeya, mkoani Mbeya, katika ziara ya kuamsha ari ya wananchi kushiriki shughuli za maendeleo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) akiangalia bidhaa ya Tomato Sauce wakati alipotembelea moja ya Kikundi cha wanawake wajasiriamali kilichopo Manispaa ya Jiji la Mbeya, mkoani Mbeya, katika ziara ya kuamsha ari ya wananchi kushiriki shughuli za maendeleo.
Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Mb) akiwa aevaa koti lililotengenezwa na wajasiliamali wadogo wakati alipotembelea moja ya Kikundi cha wanawake wajasiriamali kilichopo Manispaa ya Jiji la Mbeya, mkoani Mbeya, katika ziara ya kuamsha ari ya wananchi kushiriki shughuli za maendeleo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...