Shirika lisilokuwa la kiserikali la faidika wote pamoja FAWOPA limetoa Elimu kwa Wadau Mbalimbali wa sekta hiyo Juu ya uandaaji wa Bajeti na kuweza kuwasilisha kwa kamati za Shule, ili kuzifanyia kazi Kwa lengo la kuondokana na migongano inayojitokeza baina ya Wazazi na Walimu.

Mratibu wa shirika hilo Baltazar Komba amesema Bado viwango vya Bajeti mashuleni haijaainisha, matokeo yake Shule Nyingi wamekuwa wakitegemea wazazi kwa ajili ya michango kabla ya Mh. Rais John Pombe Magufuli kukataza Michango yoyote Mashuleni.

Aidha katika Ufuatiliaji uliofanywa na Kamati ya FAWOPA ndani ya Manispaa ya Mtwara Mikindani imebaini kuwa Halmashauri haina Bajeti maalum ya Elimu zaidi ya Bajeti kutoka Serikali Kuu.

Lengo la mkutano huo ni kuhakikisha manispaa hiyo inapiga hatua katika suala la elimu kutokana mkoa was Mtwara kuwa nyuma katika Ufaulu ukilinganisha na mikoa mwingine.
 Pichani ni mratibu wa shirika lisilokuwa la kiserikali la faidika wote pamoja FAWOPA iliyopo Mkoani  Mtwara  Baltazar Komba akizungumza na wadau mbali mbali wa elimu juu ya Uboreshwaji wa Elimu mkoani Humo.
Mshauri wa Mambo ya Kisheria FAWOPA Marythereza Namangi akitoa mafunzo kwa Wadau Mbalimbali wa Elimu Juu ya uandaaji wa Bajeti katika mashule kama Moja ya dhana ya Uwazi na Uwajibikaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...