Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

SERIKALI ya Tanzania imesaini makubaliano na Serikali ya Israel ya ujenzi wa kitengo cha dharula na tiba ya mifupo katika hospitali ya Benjamini mkoani Dodoma.

Akizungumza baada ya kusaini makubaliano hayo leo jijini Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk.Otilia Gowelle amesema kuwa ujenzi wa kitengo hicho utasaidia katika utoaji wa huduma za afya zilizo bora.

Amesema kitengo hicho kitajengwa na Serikali ya Israel ikiwa ni pamoja na madaktari nchini kujengewa uwezo katika utoaji wa huduma katika kitengo hicho.Dk. Gowelle amesema kuwa ushirikiano uliopo kati ya Israel na Tanzania ni uhusiano imara katika kusaidia utoaji huduma katika sekta ya afya.
.Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk. Otilia Gowelle akisaini makubaliano na Naibu Balozi wa Israel Nchini, Michael Baror ya ujenzi wa kitengo cha dharula na tiba ya mifupa katika Hospitali ya Benjamini mkoani Dodoma, leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk. Otilia Gowelle akibadilishana hati ya makubaliano na Naibu Balozi wa Israel Nchini, ,Michael Baror ya ujenzi wa kitengo cha dharula na tiba ya mifupa katika Hospitali ya Benjamini mkoani Dodoma, leo jijini Dar es Salaam.
Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Dk. Otilia Gowelle na Naibu Balozi wa Israel Nchini,Michael Baror pamoja na watendaji mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kusaini makubaliano ya ujenzi wa kitengo cha dharula na tiba ya mifupa katika Hospitali ya Benjamini mkoani Dodoma, leo jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...