Katibu Tawala wilaya ya Temeke, Ndugu Hashim Komba akikabdhi  mfano wa hundi kwa mshindi wa mchezo wa bahati nasibu wa Tatumzuka  Enirisha Kilango mapema leo kwenye ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Temeke.Enirisha Kilango ambaye ni Mkazi wa Temeke Mikoroshini anaejishughulisha na biashara zake ndogo ndogo alijishindia milioni 50 mwishoni mwa wiki
Enirisha Kilango ambaye ni Mkazi wa Temeke Mikoroshini anaejishughulisha na biashara zake ndogo ndogo akizungumza mapema leo mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) ndani ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Temeke,kufuatia ushindi wake wa kujinyakulia milioni 50 mwishoni mwa wiki katika mchezo huo wa kubahatisha.
 Katibu Tawala wilaya ya Temeke, Ndugu Hashim Komba akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa wilaya ya Temeke, mbele ya Waandishi wa habari  (hawapo pichani) mapema leo,kabla ya kukabidhi mfano wa hundi kwa mshindi wa mchezo wa bahati nasibu wa Tatumzuka kwa mshinidi aliyejinyakulia Enirisha Kilango aliyejishindia milioni 50 mwishoni mwa wiki .

Ndugu Komba amewashukuru Tatumzuka kwa kuendelea kuwawezesha wananchi wa wilaya hiyo ya Temeke kupitia mchezo huo wa bahati nasibu,kwa kumpata mshindi mwingine ndani ya wilaya hiyo kwa mara nyingine tena,Komba amewasisitizia wananchi wake kuendelea kucheza zaidi na zaidi kwani mchezo ambao upo kisheria na hauna makando kando yoyote,ukishinda umeshinda kweli na fedha zako unakabidhiwa.

Mh Komba aliongeza kuwa kama Tatumzuka itawapatia shilingi Milioni Tano ambayo  imepatikana mara baada ya mshindi huyo kupatikana,basi watazitumia fedha hizo kuimarisha suala la ulinzi na usalama, tutakwenda kujenga kituo cha polisi na kuzitumia fedha hizo kununua mabati ili kukamilisha ujenzi wa vituo hivyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...