*Philison Mdee aongoza kwa wavulana,  Ellizabeth  Mangu aongoza wasichana

*Wengine 265 matokeo yafutwa, yumo aliyeandika matusi kwenye majibu


 Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
SHULE ya Sekondari ya St.Francis Girls imeongoza kwa kushika nafasi ya kwanza kitaifa katika matokeo ya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2017.

Akitangaza  sekondari ambazo zimeshika nafasi za juu kwenye matokeo hayo, leo jijijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk.Charles Msonde amesema nafasi ya pili imechukuliwa na sekondari ya Feza Boys na nafasi ya tatu sekondari ya Kemebos.

Wakati nafasi ya nne imeshikiliwa na sekondari ya  Bethel Saabs Girls, nafasi ya tano sekondari ya Anuarite, nafasi ya sita sekondari ya  Marian Gilrs huku nafasi ya saba ikishikiliwa na sekondari ya Canossa, wakati nafasi ya nane imechukuliwa na sekondari ya Feza Girls, nafasi ya tisa sekondari ya Marian Boys na nafasi ya 10 sekondari ya Shamsiye Boys

WALIOONGOZA 10 BORA KITAIFA
Kwa upande wa wanafunzi ambao wameshika nafasi ya kwanza hadi ya kumi kitaifa kwenye matokeo hayo, Dk.Msonde alisema nafasi ya  kwanza imeshikwa na mwanafunzi Philison Mdee(Marian Boys), wakati nafasi ya pili imeshikwa na Eliza Mangu(Marian Girls), nafasi ya tatu
Ana Mshana(Marian Girls)

Ametaja nafasi ya nne imeshikwa na Emanuel Makoye(Ilboru), nafasi ya tano Lukelo Luoga(Ilboru), nafasi ya sita Fuad Thabit(Feza Boys), nafasi ya saba Godfrey Mwakatage(Uwata), nafasi ya nane Baraka Mohamed(Angeles), nafasi ya tisa Lilian Moses(Marian Girls) na nafasi ya kumi kitaifa imechukuliwa na Everine Mlowe(St. Francis Gr)

WAVULANA 10 BORA KITAIFA 
Akitangaza walioshika nafasi ya kwanza hadi ya 10 kitaifa kwa mujibu wa Dk.Msonde ni Philison Mdee(Marian Boys), nafasi ya pili Lameck Makoye(Ilboru), nafasi ya tatu Tadei Luoga(Ilboru), nafasi ya nne Fuad Thabit (Feza Boys).

Wakati nafasi ya tano ni  Godfrey Mwakatage(Uwata),nafasi ya sita  Baraka Mohamed(Angeles),nafasi ya saba  Noel Shimba(Marian Boys), nafasi ya nane ni Patrick Robert(Mzumbe), nafasi ya tisa Robison Eliona(ILboru) na nafasi ya 10 bora kitaifa imechukuliwa na mwanafunzi Harrison Simkoko (Mzumbe)


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...