Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji Jumaa Aweso amesema Serikali ya Rais Magufuli kupitia Wizara ya Maji na Umwagiliaji imetoa kipaumbele kwa viwanda vya ndani vinavyozalisha bidhaa zinazotumika kutekeleza miradi mikubwa ya maji inayoendelea kujengwa nchini kote.
Aweso ametoa kauli hiyo mjini Kahama alipotembelea kiwanda cha Kahama Oil Mills, mkoani Shinyanga ambacho moja ya shughuli zake ni kutengeneza mabomba na vifaa mbalimbali vinavyotumika kutekeleza miradi ya maji na kutoa angalizo kwamba ni lazima viwanda vya ndani vizingatie ubora wa bidhaa zao na kukidhi mahitaji halisi ya miradi yote ya maji nchini.
‘‘Hatuna sababu ya kutotumia bidhaa zinazozalishwa na viwanda vyetu vya ndani, maadamu vinazingatia ubora wa bidhaa inazozalisha na kukidhi mahitaji ya nchi yetu. Serikali ya Rais Magufuli imetoa kipaumbele kwa wazalendo nchini, hivyo tumieni fursa hii na kutomuangusha,’’ alisema Aweso.
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso akipokea maelekezo kutoka kwa Meneja Mradi wa Kiwanda cha Kahama Oil Mills, Jiten Divecha (kulia) ambacho moja ya shughuli zake ni kuzalisha vifaa vya maji kilichopo wilayani Kahama, mkoani Shinyanga alipotembelea kiwandani hapo.
 Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Jumaa Aweso akihakiki ubora wa maji yanayozalishwa na mradi wa pamoja (Joint Water Partnership Project) unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu na halmashauri za wilaya ya Shinyanga na Msalala kwa mkoa wa Shinyanga na Nyangh'wale kwa Mkoa wa Geita.
Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Kakola ambacho ni miongoni mwa vijiji 13 vitakavyonufaika na mradi wa pamoja (Joint Water Partnership Project) unaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu na halmashauri za wilaya ya Shinyanga na Msalala kwa mkoa wa Shinyanga na Nyangh'wale kwa Mkoa wa Geita.
 Baadhi ya mabomba yanayozalishwa na Kiwanda cha Kahama Oil Mills kilichopo wilayani Kahama, mkoani Shinyanga.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...