Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaasa wavuvi wanaozunguka ziwa Rukwa kuhakikisha wanatafuta ardhi kwaajili ya kilimo, biashara pamoja na ufugaji katika kipindi cha kunzia mwezi wa kwanza hadi wanne kila mwaka ili kuwaacha samaki wa ziwa hilo kuzaliana.

Amewaasa kutotegemea shughuli moja tu kwaajili ya kuwaingizia kipato, “Wavuvi msitegemee kuvua tu, jishughulisheni na kazi nyingine za kuwaingizia kipato kama vile kilimo, biashara pamoja na ufugaji, hatufungi kambi hizi kwaajili ya kipindupindu tu lakini pia ili kuweza kuwaacha samaki wazaliane katika kipindi cha kuanzia mwezi wa kwanza hadi wanne,”

Ameyasema hayo alipofanya ziara kwenye kambi ya Nankanga iliyopo katika Kijiji cha Solola Wilayani Sumbawanga ili kujionea hali halisi ya maisha ya wavuvi katika kambi zisizo rasmi na namna ya kuweka mpango salama wa kuweza kuwaepusha na ugonjwa wa kipindupindu ulioenea katika makambi hayo yanayozunguka ziwa Rukwa. 

Tangu ugonjwa huo uingie Mkoani Rukwa tarehe 15/11/2017 tayari watu 210 wanaugua ugonjwa huo na watu nane wamepoteza maisha wote wakiwa wanatokea katika makambi hayo yasiyo rasmi ambapo hadi sasa kambi zisizo rasmi zaidi ya tisa zimefungwa huku zoezi hilo likitegemewa kuendelea hadi hapo Mwezi wa tano.

Nae Diwani wa kata ya Nankanga kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dk. Khalfan Haule amesema kuwa katika kambi hiyo kuna watoto 270 walio na umri chini ya miaka 7 ambao wamekosa kwenda shule na hivyo wananchi kujenga madarasa mawili ya shule shikizi katika kitongoji kilichopo Km 9 kutoka kwenye kambi hiyo yaliyofikia usawa wa linta na kumuomba Mkuu wa Mkoa kuwaunga Mkono jambo lililompelekea Mh. Wangabo kutoa bati 50 na kuitaka Halmashauri kuongezea bati 50 ili kukamilisha ujenzi huo.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo akiwaasa wavuvi wa kambi ya Nankanga kujishughulisha na kilimo hasa katika kipindi cha mwezi wa kwanza hadi wa Nne kila mwaka pindi shughuli za uvuvi zinapofungwa ili kuwaacha samaki wazaliane na kutunza Ziwa lisipotee kwa faida ya vizazi vijavyo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...