NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Mtwara

SEMINA ya siku tano ya waandishi wa Habari za Uchumi, Biashara na Fedha iliyoandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania, Idara ya Uhussiano na Itifaki, imemalizika leo Februari 5, 2018 mkoani Mtwara.

Katika simian hiyo iliyofunguliwa mwanzoni mwa wiki na Naibu Gavana wa Benki Kuu anayeshughulikia Utawala na Udhibiti wa Ndani (AIC), Bw. Julian Raphael Banzi, waandishi hao wamejifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya mfumo mpya wa kuandaa Sera ya Fedha, (Financial Monetary Policy), mapitio ya maendeleo ya uchumi nchini, kikanda na dunia, mifuko ya dhamana kwa wajasiriamali na dhamana za serikali. 

Mambo mengine ambayo waandishi hao kutoka vyombo mbalimbali vikiwemo, Redio, Luninga, Magazeti na Blogs ni kanuni mpya za usimamizi wa bureaux de change, usimamizi wa mabenki na taasisi za fedha na dhamana kwa mikopo ya nyumba (Mortgage Finance). 
Kaimu Mkurugenzi wa BoT, Tawi la Mtwara, Bi. Leticia Rweyemamu, akitoa hotuba ya kufunga semina ya sikju tano ya waandishi wa habari za Uchumi, Biashara na Fedha, kwenye makao makuu ya tawi hilo Mkoani Mtwara leo Ijumaa Februari 9, 2018.
Kaimu Meneja wa Idara ya Uhusiano na Itifaki, BoT, Bi. Vicky Msina, akizungumza wakati wa hafla ya ufungaji wa semina hiyo.
Dkt. Suleiman Missango, Meneja Msaidizi-Idara ya Utafiti, Kurugenzi ya Sera za Uchumi na Utafiti, BoT, akiwasilisha mada kuhusu Government securities (Government Date Securities) , mwishoni mwa semina hiyo leo Februari 9, 2018.
Baadhi ya washiriki wakifurahia hotuba ya mgeni rasmi.
Meneja Msaidizi, Dawati la Kutatua Malalamiko ya wateja wa mabenki na taasisi za fedha, Benki Kuu ya Tanzania, (BoT) Bw.Ganga Ben Mlipano, akitambulishwa kwa wana semina kabla ya kuwasilisha mada ya mafanikio na changamoto za dawati hilo.
Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na wawezeshaji na wana semina mwishonin mwa semina hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...