Bondia wa Kimataifa Francis Cheka anatarajia kupigana na Bondia Arney Tinampay Kutoka Nchini Ufilipino katika Pambano la raundi 10 litakalofanyika katika Uwanja wa Umoja Nangwanda Sijaona Mkoani Mtwara mwanzoni mwa mwezi wa Nne.

Kwa mara ya Kwanza Bondia Franciss Cheka anapigana Mchezo wa Kimataifa wa Kutetea Ubingwa wa Mkanda wa UBO wa kilogram76 katika Mkoa wa Mtwara,ambapo tayari ameanza Kufanya maandalizi ya Mazoezi tayari kwa Pambano hilo.AKiongea na waandishi wa habari Promota Jay Msangi anasema Bondia Kutoa Ufilipino anatoka katika Historia ya mabondia wakubwa.

“Bondia huyu anahistoria anatokea katika kambi ya Man Pacquiao na anayemfundisha  aliwah pia kumfundisha Pacquiao na ni Bondia mwenye kushika daraja la pili katika Nchi ya Ufilipino kenye uzito wa Kilogram 76 na hivyo unaweza kuona kwa Francis Cheka anakutana na Bondia Mwenye uwezo mkubwa”alisema Promota Jay Msangi.

Naye Fransis Cheka anasema anajiamini licha ya kuwa hamfahamu Bondia huyo Kutoka Ufilipino lakini uwezo wake ni mkubwa kupigana na bondia yeyote wa kiwango chake.

“Sifahamu Uwezo wa Mfilipino lakini najifahamu uwezo wangu kwa sababu nimeshakuwa Bingwa wa Dunia na hivyo nawahakikishia Watanzania hususani wakazi wa mkoa wa Mtwara nitafanya vizuri,Simfahamu huyo Bondia lakini nitakapokutana naye Ulingoni tutafahamiana Hapo Hapo”Alisema ChekaCheka.

Wakati huo huo Bondia Francis Cheka amekabidhiwa Ubalozi wa Kuitangaza Eneo la Mikindani ambalo lina majengo ya Kihistoria. 
 Mzee Mohammed Kidume Akimsimika Ubalozi wa Mikindani Bondia Francis Cheka katikati kwa lengo la Kutangaza historia ya Majengo ya Kale ambayo yalitumiwa na Wakoloni.
Bondia Francis Cheka akiwa na wazee wa Mikindani Mara baada ya kukabidhiwa Ubalozi wa kutangaza Hotel ya Old Boma Iliyopo Mkoani Mtwara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...