Na Humphrey Shao , Globu ya Jamii
Ilikuwa Usiku wa February 17 mwaka huu msanii wa Muziki wa Bongo Fleva Aslay Isihaka alibadilisha historia ya muziki katika Maisha yake kwa kufanya shoo kubwa ya Mapenzi na Muimbaji Mwenzie Nandy ambae wameshirikiana katika nyimbo nyingi.
Licha ya usiku huo kufikiriwa kuwa wa nyimbo za Mahaba mambo yalikwenda tofauti kwa nusu saa nzima pale Aslaya alipopanda jukwaani na kibao cha “Angekuwepo” wimbo ambao aliumba kwa ajili ya kumkumbuka Mama yake Mzazi.
Aslay ambaye aliimba kisha kuishia kati na kwenda kumsogelea Mama Mzazi wa Nandy na kusema kuwa “natamani muda huu Mama yangu muda huu angekuwa hapa lakini sio mapenzi yangu...Natamani namimi ningekuwa kama Nandy naimba Mama yangu anaona. Hivyo nikuombe Mama Nandy kuanzia leo uwe mama yangu hili niweze kupata faraja kama anayopata mwanao” alisema Aslay.
Maneno yaliteka hisia za watu wengi na kumfanya Mama yake Nandy kuamka na kwenda kucheza na Aslay na kufanya watu wengi kuinuka kwenda kumwambia mwanamuziki huyo aendelee kuimba na kuacha kulia.
Aslay ambaye aliendelea kuimba wimbo huo huku akiwa amekaa chini kwa  huzuni na kutengeneza simanzi kubwa ndani ya ukumbi wa Escape One kwa zaidi ya Dk 30. Wengi walilengwa na machozi na kukubali kuwa Mama ni wa muhimu kuliko kitu chochote maishani.
 Aslay Isihaka akionyesha kidole juu kumshukuru Mungu kwa yote yaliyotekea katika maisha yake.
 Aslay akimuomba   Mama yake Nandy  kuwa Mama yake wa kumlea wakati anaimba wimbo wake angekuwepo
 Aslay akicheza na Mama yake Nandy  mara baada ya kukubali kuwa Mama Mlezi
 Mmoja wa Mashabiki wakinyamazisha Aslay asilie wakati anaimba wimbo angekuwepo
Mashabiki wa muziki wakiwa wamesimama kwa huzuni wakati Aslay akiimba wimbo huo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...