Hali ya "Sanda Mkobani" ilivyokuwa wakati wa kuvuka mto Kilombero mkoani Morogoro kabla ya ujenzi wa daraja.
Ujenzi wa Daraja la Mto Kilombero uliopangwa kukamilika mwezi Februari 2017, sasa umekamilika kwa 100% na liko tayari kuzinduliwa.  Daraja hilo linalounganisha wilaya mbili za mkoa wa Morogoro (Ulanga na Kilombero) pamoja na Mkoa wa Ruvuma, litaokoa maisha ya wananchi wa wilaya hizo ambao katika kipindi chote cha mwaka walikuwa wakipata shida kuvuka mto huo huku shughuli za usafirishaji wa mazao ya mpunga, ufuta, mahindi, ufugaji na madini zitarahisishwa,  kuongeza pato na kukuza uchumi wa Taifa.Pia kukamilika kwa daraja la Mto Kilombero kutarahisisha usafiri kutoka Dar kwenda Songea – Ruvuma ambapo ni mbali mfupi sana kwa kupitia Mikumi-Ifakara-Mahenge mpaka Songea kuliko kupitia Iringa-Njombe mpaka Songea.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Baba yangu Mzee Lyaheja Alizama na Bai la MOretc1988 alipona,, Rafiki Yangu Omar aliuwa askari poice alifariki hapa 1999

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...