Mchungaji wa Mji Mtakatifu na kazi nyingine za Palestina na Jordan Theophilus III, kwa niaba ya wachungaji na viongozi wote wa Makanisa ya Jerusalemu (Makanisa ya Kigiriki, Kikatoliki na Kiarmenia),katika hatua ambayo haijawahi kutokea, Jumapili iliyopita ametangaza kulifunga Kanisa hilo la Ufufuo lililopo Jerusalemu ya kale hadi itakapotolewa taarifa nyingine,ikiwa ni kutokukubaliana na kupinga kwao na sera za utawala wa kivamizi wa Israeli dhidi ya Makanisa na kuyataka yalipe kodi.

Hayo yamesemwa wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika kiwanja cha Kanisa hilo la Ufufuo,ikiwa ni kupinga vitendo vya utawala wa kivamizi dhidi ya makanisa hayo. Kwani utawala huo hivi karibuni umeyataka Makanisa hayo ya Jerusalemu yalipe kodi ya mali ijulikanayo kama"Arnona",yenye thamani ya shekel milioni kila mwaka, huku ukiingilia mali za Kanisa la Orthodox la Kirumi kwa lengo hilohilo.

Nao Viongozi wa Makanisa ya Jerusalemu katika mkutano wa waandishi wa habari, wametoa tamko wakisisitiza ya kwamba,”Kuyatoza kodi Makanisa mjini Jerusalemu ni ukiukwaji wa mikataba yote iliyopo na wajibu wa kimataifa unaodhamini haki za Makanisa na mambo yake maalumu." Tamko hilo limesisitiza kuwa, hatua hiyo ni "jaribio la kudhoofisha uwepo wa Kikristo katika jiji hilo," Huku likionya kuupitisha mpango wa kamati ya wizara iliyo chini ya utawala wa kivamizi wa Israeli wa kutoza kodi kwa Makanisa mjini Jerusalemu,ambao unafanyika kupitia kuchukua kwa nguvu ardhi ya Makanisa hayo yaliyo mjini hapo.
Serikali ya Palestina imeizingatia hatua ya utawala wa kivamizi kutoza kodi nyumba za ibada yakiwemo makanisa, kuwa ni uadui mpya dhidi ya wananchi na maeneo yake matakatifu, jambo lililopelekea kufungwa kwa kanisa la Ufufuo lililopo katika mji mkuu unaokaliwa kimabavu. Huku ukiuchukulia uadui huo mpya kuwa unalenga mji wa Jerusalemu na taifa letu lote la kiarabu la kipalestina pia unagusa maeneo yake matakatifu, huku likionya juu ya madhara makubwa yanayoweza kunyakua ardhi za makanisa.

Serikali imeomba kuingilia kati kwa haraka kwa jumuiya ya kimataifa ili kusitisha vitendo hivyo vya Israeli, ambavyo vinahesabiwa kuwa ni mashambulizi mabaya ya mikataba,makubaliano na desturi zote za kimataifa, vinavyodhamini uwepo wa uhuru wa kuabudu na kuheshimu utakatifu wa sehemu za kidini,katika hali yoyote na popote. Serikali pia imetoa wito maalumu kwa ulimwengu wa kikristo na kiislamu, wa kuchukua hatua stahiki kwa ngazi zote ili kuzuia vitendo vya kivamizi, vinavyolenga kwa kiwango sawa sehemu takatifu za kikristo na kiislamu.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...