Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kushoto) akiteta jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba wakati wa mkutano wa tano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Maliasili na Mazingira wa Nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki uliohitimishwa leo katika ukumbi wa EAC jijini Arusha. Mkutano huo ulilenga kujadili na kusaini makubaliano mbalimbali ya namna bora ya kusimamia sekta hizo katika nchi wanachama. 
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba (kulia) akisaini baadhi ya makubaliano yaliyofikiwa katika mkutano wa tano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Maliasili na Mazingira wa Nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki uliohitimishwa leo katika ukumbi wa EAC jijini Arusha. Mkutano huo ulilenga kujadili na kusaini makubaliano mbalimbali ya namna bora ya kusimamia sekta hizo katika nchi wanachama. Wanaoshuhudia ni Mawaziri wa Mazingira kutoka Uganda na Kenya.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia), Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba (wa pili kulia) na Balozi wa Sweden nchini Tanzania, Bi. Katerina Rangnitt wakiangalia baadhi ya michoro ya katuni za kuhamasisha uhifadhi wa mazingira muda mfupi baada mkutano wa tano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Maliasili na Mazingira wa Nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki uliohitimishwa leo katika ukumbi wa EAC jijini Arusha. Mradi huo ya katuni unafadhiliwa na Serikali ya Sweden kwa ushirikiano na Serikali ya Tanzania.
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla (kulia) na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba wakimsikiliza mmoja ya wachora katuni za kuhamasisha uhifadhi wa mazingira muda mfupi baada mkutano wa tano wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Maliasili na Mazingira wa Nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki uliohitimishwa leo katika ukumbi wa EAC jijini Arusha. Mkutano huo ulilenga kujadili na kusaini makubaliano mbalimbali ya namna bora ya kusimamia sekta hizo katika nchi wanachama. 
 Picha ya pamoja ya baadhi ya wajumbe wa mkutano huo.(PICHA ZOTE NA HAMZA TEMBA-WMU)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...