Na,Joel Maduka,Geita. 


NAIBU Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo amesema Serikali ya Awamu ya Tano haiko tayari kuona mtu akilalamika ,kunyanyaswa au kunyimwa haki yake.

Ametoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Nyakabale, Kata ya Mgusu wilayani Geita wakati wa ziara yake ya siku mbili mkoani humo ya kuzungukia maeneo ya uchimbaji na kusikiliza kero za wananchi walizunguka kwenye baadhi ya maeneo ya mgodi wa Geita(GGM).

Hatua hiyo ya Naibu Waziri Nyongo imekuja baada ya kusikia malalamiko mengi kutoka kwa wananchi kuhusu mgodi wa GGM kushindwa kuwalipa fidia kwa muda mrefu licha ya kuwepo kwa maagizo mengi  yaliyotolewa na  baadhi ya viongozi ambao wamekuwa wakifika mkoani humo.

 Amesema mtu mwingine yuko tayari kuona Mtanzania mwenzake akikandamizwa ilimradi yeye aendelee kulinda maslahi yake binafsi, na kwamba miaka hiyo imeshapita na muda uliopo kwa sasa ni kufanya kazi za kuwatumikia wananchi ambao ni wanyonge.
Naibu waziri wa madini Stanlaus Nyongo Akizungumza na Wakazi Wa Kijiji Cha Nyakabale wakati wa ziara yake Mkoani Geita. 
Naibu waziri wa madini Stanlaus Nyongo akishiriki zoezi la kupanda mawe ya dhahabu. 
Naibu waziri wa madini Stanlaus Nyongo akizungumza na diwani wa kata ya Mgusu Patory Ruhusa. 
Naibu Waziri Akimsikiliza Pili Mwaluko Anaefanya Kazi Ya Uchenjuaji Madini kwenye mtaa wa Nyakabale. 
Wananchi wakiwa kwenye Mkutano wa pamoja na Naibu Waziri wa madini Stanlaus Nyongo.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...