Ubalozi wa Tanzania wa Riyadh nchini Saudi Arabia hivi karibuni ulishiriki katika maonyesho ya Travel and Tourism Pioneers Forum 2018 mjini Riyadh. Maonyesho haya ya kimataifa yaaliandaliwa na Al Awasat Expo chini ya udhamini wa MwanaMfalme HRH Prince Dr. Saif Al Islam. Maonyesho haya yalizishirikisha taasisi mbalimbali zinazohusika na utalii ndani na nje ya Saudi Arabia.
Ubalozi wa Tanzania ulishiriki na kufanikiwa kutangaza vivutio mbalimbali vya utalii vilivyopo nchini ikiwa ni pamoja na kukutana na mawakala wa utalii, tour operators, travel agencies na makampuni ya kutangaza utalii.
 Baadhi ya wananchi waliotembelea banda la Tanzania katika maonyesho ya Travel and Tourism Pioneers Forum 2018 mjini Riyadh nchini Saudi Arabia.
Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Hemedi Iddi Mgaza(kushoto) akizungumza na Mwanamfalme HRH Prince Dr. Saif Al Islam bin Saud bin Abdel Aziz Al Saud alipotembelea banda la Tanzania.
Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Hemedi Iddi Mgaza(katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja  na wahudumu wa banda la Tanzania wakati wa maonyesho ya Travel and Tourism Pioneers Forum 2018.
 Wananchi wakiwa kwenye banda la Tanzania walivutiwa na taarifa walizopata na pia kuchukua vipeperushi vyenye taarifa kuhusu Tanzania.
Wakinamama walikuwa ni miongoni mwa watu waliotembelea banda la Tanzania kwenye maonyesho ya Travel and Tourism Pioneers Forum 2018 mjini Riyadh nchini Saudi Arabia.
Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Hemedi Iddi Mgaza(wa pili kushoto) akifanya mazungumzo na wananchi waliotembelea banda la Tanzania ili kupata taarifa za kina kuhusu masuala mbalimbali Tanzania kwenye maonyesho ya Travel and Tourism Pioneers Forum 2018 mjini Riyadh nchini Saudi Arabia.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...