WAZIRI
wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selemani Jafo amemtaka mkandarasi wa
kampuni ya Medes Company Limited na Millenium Master Builders (T)
Limited anayejenga daraja la Chipanga wilayani Bahi, kukamilisha ujenzi
wa daraja hilo ifikapo mwezi Julai, mwaka huu bila visingizio vyovyote.
Akikagua ujenzi wa daraja hilo, Jafo amesema awali kazi ya ujenzi wa Daraja hilo ilitarajiwa kukamilika mwanzoni mwa mwezi Aprili mwaka huu lakini kutokana na Mvua zilizokuwa zikinyesha amewaelekeza kukamilisha ifikapo Julai mwaka huu.
Jafo amewaagiza wakala wa barabara vijijini na mijini (TARURA) kukaa na mkandarasi kukubaliana tarehe ya mwisho ya kukamilika kazi hiyo lakini kinachotakiwa ifikapo Julai mwaka huu daraja hilo liwe limekamilika.
Amebainisha kuwa daraja hilo ni kiunganishi cha kata ya Chipanga na Makao makuu ya wilaya ya Bahi na ujenzi wake unagharimu kiasi cha Sh. bilioni 2.11.
Akizungumza katika mkutano wa hadharana wananchi wa Chipanga, Waziri Jafo amewataka wananchi hao kuacha tabia ya kupitisha ng'ombe na majembe ya ng’ombe kwenye barabarani zinazojengwa kwa kuwa wanasababisha uharibifu wa barabara.
Amesema serikali haiwezi kuvumilia uharibifu wowote wa miundombinu ambayo inagharimu gharama kubwa.
Akikagua ujenzi wa daraja hilo, Jafo amesema awali kazi ya ujenzi wa Daraja hilo ilitarajiwa kukamilika mwanzoni mwa mwezi Aprili mwaka huu lakini kutokana na Mvua zilizokuwa zikinyesha amewaelekeza kukamilisha ifikapo Julai mwaka huu.
Jafo amewaagiza wakala wa barabara vijijini na mijini (TARURA) kukaa na mkandarasi kukubaliana tarehe ya mwisho ya kukamilika kazi hiyo lakini kinachotakiwa ifikapo Julai mwaka huu daraja hilo liwe limekamilika.
Amebainisha kuwa daraja hilo ni kiunganishi cha kata ya Chipanga na Makao makuu ya wilaya ya Bahi na ujenzi wake unagharimu kiasi cha Sh. bilioni 2.11.
Akizungumza katika mkutano wa hadharana wananchi wa Chipanga, Waziri Jafo amewataka wananchi hao kuacha tabia ya kupitisha ng'ombe na majembe ya ng’ombe kwenye barabarani zinazojengwa kwa kuwa wanasababisha uharibifu wa barabara.
Amesema serikali haiwezi kuvumilia uharibifu wowote wa miundombinu ambayo inagharimu gharama kubwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...