WAZIRI  wa Nchi ofisi ya Rais Tamisemi  Selemani Jafo amesema hawezi kuwavumilia hata kidogo baadhi ya wawekezaji ambao wamekuwa na tabia ya  kufanya  udang’anyifu kwa wananchi kutokana na kuchukua maeneo makubwa ya ardhi pasipo kuyaendeleza mpaka yanapelekea kuwa mashamba pori hivyo ameagiza yarudishwe katika mikono ya serikali za vijiji ili wananchi wenyewe waweze kuyaendeleza katika shughuli nyingine za kimaendeleo.

Jafo ametoa kauli hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi kwa wananchi wa kijiji cha Kimara Misale kilichopo kata ya Mafizi katika halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe ambapo amekwenda kwa ajili ya kuweza kujionea  na kutembelea miradi mbali mbali ya maendeleo pamoja na kuweza kusikiliza changamoto ambazo zinawakabili wananchi wa jimbo lake.

Amesema kumekuwepo na wimbi kubwa la mashamba pori katika baadhi ya maeneo  ambayo kwa kipindi cha muda mrefu  yametelekezwa hivyo  ameahidi kulivalia njuga suala hilo kwa lengo la kuweza kuwapa fursa wananchi waweze kurudishiwa maeneo yao ambayo yamechukuliwa na watu wachache ambao wameshindwa kabisa  kuyaendeleza kama inavyostahili.
 Waziri wa nchi ofisi ya Rais Tamisemi Seleman Jafo akizungumza na wananchi wa kijiji cha  kimara misale iliyopo kata ya Mafizi Wilayani Kisarawe wakati wa ziara yake ya kikazi kwa ajili ya kukagua miradi mbai mbai ya maendeleo na kuweza kusikiliza kero na changamoto zinazowakabili wananchi ii kuweza kuzitafutia ufumbuzi.
Baadhi ya viongozi wa halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani wakiwa katika mkutano wa adhara kumsikiliza Waziri jafo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kutembelea na kujionea miradi mbai mbali ya kimaendeleo inayotekelezwa na serikali kwa kushirikiana na nguvu za wananchi wenyewe.(PICHA  ZOTE NA VICTOR MASANGU)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...