March 2018

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaomba viongozi wa dini popote walipo wahakikishe wanaipigania na kuilinda amani kwa kila hali ikiwa ni pamoja na kupambana na viashiria vya uvunjifu wa amani. 
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Machi 31, 2018) kwenye Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) uliofanyika katika ukumbi wa Pius Msekwa mjini Dodoma, ambapo amesisitiza kuwa ni muhimu wasaidizi wa Mufti wakasimamia suala hilo. 
“Dini ni taasisi muhimu sana kwa maisha yetu ya kila siku ndio maana Serikali inaheshimu na kuzitambua dini zote kutokana na mchango wake mkubwa katika amani ya nchi yetu. Niwaombe viongozi wangu popote mlipo muilinde amani yetu” 
Waziri Mkuu amesema amani ni miongoni mwa neema kubwa sana kwa binadamu na ndio maana wote wanamtambua Mwenyezi Mungu, hivyo wasiruhusu mtu au kikundi chochote kujaribu kuchafua na kuharibu amani iliyopo nchini. 
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewasisitiza viongozi Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) wahakikishe kuwa chombo hicho kinaendelea kuwaunganisha waislamu bila ya kujali makabila yao, rangi zao au madhehebu yao.  
Waziri Mkuu amesema Mufti wa Tanzania Sheikh Aboubakar bin Zubeiry ambaye ndiye kiongozi wa Waislamu nchini mara zote amekuwa akisisitiza jambo hilo na kuwataka waislamu popote walipo watambue kuwa hicho ni chombo chao. 
“Ni muhimu sana kwa ninyi wasaidizi wa Mufti mlio kusanyika hapa muhakikishe mnalisimamia hili katika maeneo yenu. Katika hili napenda kuwahakikishia kuwa Serikali yenu iko pamoja Mheshimiwa Mufti kutekeleza nia hiyo njema.” 
Amesema ahadi ya Rais Dkt. Magufuli ni kuwa Serikali anayoiongoza ipo tayari kusikiliza maoni, ushauri na  mapendekezo yeyote kutoka kwa viongozi wa dini . ‘Milango iko wazi saa zote ‘ 
Ameongeza kuwa yeye si mtaalamu sana kama walivyo Masheikh hao lakini anakumbuka maneno ya Mwenyezi Mungu ndani ya Qur’ani sura Al Imran aya ya 103 yanayosema “ Shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu nyote na wala msifarakane” 
Mkutano huo umehudhuriwa na  Sheikh Mkuu wa Mufti wa Tanzania Sheikh Zubeir, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, wajumbe wa Baraza la Ulamaa, Masheikh na viongozi wa BAKWATA wa mikoa na wilaya zote Tanzania.
 Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akilakiwa na Mufti wa Tanzania Sheikh Aboubakary bin Zubeiry alipowasili kufungua  mkutano mkuu wa BAKWATA kwenye ukumbi wa Msekwa mjini Dodoma.
 Mufti wa Tanzania Sheikh Aboubakary bin Zubeiry akiongea kabla ya kumwalika Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa  kufungua  mkutano mkuu wa BAKWATA kwenye ukumbi wa Msekwa mjini Dodoma.
  Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akihutubia wakati anafungua mkutano mkuu wa BAKWATA kwenye ukumbi wa Msekwa mjini Dodoma.
   Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akihutubia wakati anafungua mkutano mkuu wa BAKWATA kwenye ukumbi wa Msekwa mjini Dodoma.
   Sehemu ya wajumbe wakimsikiliza Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akihutubia wakati anafungua mkutano mkuu wa BAKWATA kwenye ukumbi wa Msekwa mjini Dodoma.
  Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa akisalimiana na wajumbe baada ya kufungua mkutano mkuu wa BAKWATA kwenye ukumbi wa Msekwa mjini Dodoma. Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
Ndugu wapendwa watanzania na marafiki wa Tanzania wote, tunasikitika kutangaza kifo cha ndugu yetu Leyla Mtumwa kilichotokea tarehe 30 March 2018 mjini London. Inasadikiwa mauti yalimkuta  baada ya purukushani na mume wake ambapo alichomwa kisu na kufariki papo hapo. 

Mwili wa marehemu bado unahifadhiwa na polisi  kwa ajili ya uchunguzi, baada ya  taratibu nyingine. Tutakujulisheni taarifa nyingine tutakayoipata haraka iwezekanavyo.

Msiba utakuwa:
CM 18 7SD

Kama desturi yetu tulionayo kama jamii tunawaomba michango yenu kwa hali na mali ili kufanikisha zoezi la kuusafirisha mwili  wa marehemu kwenda Arusha,Tanzania. 

Account details: RMI Kieti 
Sort code 20-36-98  
Account no 63049248 
Bank. 

Kwa taarifa zaidi wasiliana na 
Malick Kieti 07787449340 .
Said John 07957542863.
Enzy Larusai 07956483352. 
Leo asubuhi nimefika alipokua akiishi msanii Man Dojo.Taarifa ya awali inaonesha kuwa eneo alilojenga kuna viwanja vitatu ambavyo vina hati na kuna watu walipewa mwaka 2003.Mwaka 2013 viwanja hivyo vikiwa havijaendelezwa,Man Dojo aliuziwa na mtu aliyedai ni mmiliki wa eneo hilo kwa Tsh milioni 3 wakimuaminisha kuwa ni mali yao.

Wenye hati wameeleza kuwa walifungua kesi na kushinda katika Baraza la ardhi la wilaya, hivyo kupata amri ya kubomoa.Baada ya yake kubomolewa, kwa sasa Man Dojo na familia yake wanalala nje.

Baada ya kuona na kusikiliza mechukua hatua zifuatazo kwa awali:-

1. Nimeelekeza Man Dojo atafute nyumba ya kujistiri yeye na mkewe eneo la Mbweni kwa kipindi cha mpito ambayo nitamlipia kwa miezi sita.

2. Nimeagiza wote waalioshiriki kumtapeli Man Dojo kwa kumuuzia kiwanja huku wakijua si mali yao wakamatwe na jeshi la Polisi haraka iwezekanavyo.Kitendo walichofanya ni jinai na lazima washughulikiwe kwa mujibu wa sheria.

3. Nimemuita Man Dojo ofisini kwangu siku ya jumanne saa 4 asubuhi na wenzie ambako tutafanya kikao na mashauriano na wataalam wa ardhi wa manispaa na uongozi wa kata ya Mbweni ili kujiridhisha kiini cha jambo hili, kupitia nyaraka zote na kuona namna tutakavyomsaidia kwa kutumia HEKIMA, BUSARA NA UBINADAMU.

4. Nimeagiza, Mkurugenzi kupitia idara ya ardhi na Mipangomiji Kinondoni kuniletea taarifa ya watu wote waliopewa viwanja kwa kuanzia na Mbweni ambao hawajaendeleza viwanja vyao hadi sasa (kama masharti ya hati yanavyowataka).

Kutoendeleza viwanja kunatoa mwanya kwa matapeli kuwatapeli wananchi wenye shida ya dhati ya ardhi ya kujenga makazi kama ilivyokua kwa ndugu yetu.Wako watu walipewa viwanja mwaka 2003 lakini hadi leo wameshindwa kusafisha na kuendeleza viwanja vyao.Badala yake viwanja hivyo vimekua vichaka na maficho ya wahalifu.

5. Siku ya jumatano wiki ijayo nitazungumza na umma juu ya nini kimejiri katika kikao changu cha jumanne na namna gani tutamsaidia na kumshauri Man Dojo.Nafahamu jinsi ilivyo taabu kujenga, nafahamu jinsi kazi ya sanaa ilivyo ngumu hadi kudunduliza na kujenga.

Lakini nawaasa wananchi wote wa Kinondoni kuchukua tahadhari na kujiridhisha kabla ya kufanya manunuzi yoyote ya kiwanja.Ni vyema kupata ushauri kwa wataalam wetu wa ardhi kabla ya kununua kiwanja na kuanza ujenzi.
Msanii Man Dojo akielezea jambo kwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Alli Hapi sambamba na kamati ya ulinzi na usalama pamoja na viongozi wa serikali ya mtaa wa Mbweni.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Alli Hapi akimsikiliza Msani  Man Dojo akielezea namba tukio la nyumba yake lilivyokuwa,mapema leo jijini Dar
 
no image
Baada ya kupata baraka zote toka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda mabingwa wa muziki wa starehe nchini The Kilimanjaro band Wana Njenje wamerudi upya pale pale Salender Club jijini Dar kuanzia Jumamosi hii ya leo Machi 31, 2018 na kila Jumamosi kuanzia saa tatu hadi majogoo kama kama kawaida yao. Usiseme hukuambiwa  Hallooo...Hallooooo..



MKurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akifafanua jambo mbele ya Maaskofu na Wachungaji wa mkoa wa jiji la Mwanza mapema leo jijini humo kuhusu upokeo na maandalizi ya tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika hapo kesho Aprili Mosi,ndani ya  uwanja wa CCM Kirumba mkoani humo.
MKurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akizungumza na Maaskofu na Wachungaji wa mkoa wa jiji la Mwanza mapema leo kwenye moja ya hoteli jijini humo,akieleza kukamilika  rasmi kwa maandalizi ya tamasha la pasaka,linalotarajiwa kufanyika hapo kesho Aprili Mosi katika uwanja wa CCM Kirumba mkoani humo.

Msama amewashukuru Maaskofu hao na Wachungaji kwa kujitoa na kuunga mkono Tamasha la Pasaka 2018,ambalo kwa mara ya kwanza linaanzia kufanyika jijini Mwanza na baadae kuhamia mkoa wa Simiyu ndani ya mji wa Bariadi April 2 ndani ya uwanja wa Halmashauri,aidha tamasha hilo litakuwa na waimbaji lukuki ambao tayari wameishatangazwa kushiriki,kuhakikisha tamasha hilo linafana.
 
Kwa upande wa Maaskofu wameipongeza Kampuni ya Msama Promotions,chini ya Mkurugenzi wake Alex Msama kwa kuupa mkoa wa Mwanza kipaumbele kwa kuleta tamasha hilo mkoani humo,Wameongeza kuwa tamasha hilo litawavuta waumini wengi na wapenzi wa muziki wa injili na kuwaleta pamoja ili kupata neno la mungu na uponyaji kwa njia ya uinjilisti wa nyimbo za injili .
katika picha kutoka kushoto ni Askofu Charles Sekelwa Mwenyekiti wa Umoja wa Makanisa Mwanza na Askofu Zenobius Isaya kutoka kanisa la Philadephia Gospel Asembly na mlezi wa Msama Promotion Kanda ya Ziwa.

Askofu Zenobius Isaya kutoka kanisa la Philadephia Gospel Asembly na mlezi wa kampuni ya Msama Promotion Kanda ya Ziwa,akitoa ufafanuzi wa namna tamasha hilo la Pasaka 2018 lilipofikia na maandalizi yake kwa ujumla,mbele ya kikao cha Maaskofu na Wachungaji kilichofanyika mapema leo jijini humo,kulia ni Mkurugenzi wa Msama Promotion Bw. Alex Msama na kushoto ni Askofu Charles Sekelwa Mwenyekiti wa Umoja wa Makanisa Mwanza.

Mmoja wa maaskofu akitoa mchango wake katika kikao hicho kilichofanyika jijini Mwanza leo.
Askofu Joyce Mangu wa kanisa la Calvary Assemblies Of God Mjini Kati jijini Mwanza akizungumza wakati akitoa mchango wake katika kuboresha tamasha hilo siku za usoni na kwamba amefurahishwa sana na ujio wa tamasha hilo kwa jiji la Mwanza.



Baadhi ya maaskofu na wachungaji wakifuatilia kikao hicho. 
 Kamishna wa Operesheni wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CF) Billy Mwakatage (kushoto), akiwa ameambatana na mwenyeji wake mmiliki wa Yatch Club Bw. Brian Fernandes (kulia), baada ya kuwasili ofisi za Yatch Club kwa ajili ya uzinduzi wa mafunzo ya uzamiaji majini kina kirefu daraja la pili kwa Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Jijini Dar es Salaam. Alipotembelea eneo hilo mapema leo asubuhi. Mafunzo haya yanayoendeshwa hapa nchini na Wakufunzi kutoka Ujerumani yana lengo la kuwaongezea Maafisa na Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji weledi katika kukabiliana na majanga ya mafuriko na kuzama kwa watu majini haswa kwenye kina kirefu.
 Kamishna wa Operesheni wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji (CF) Billy Mwakatage (wa pili kushoto), akiwa na wakufunzi kutoka nchini Ujerumani na Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji. Wakati wa  uzinduzi wa mafunzo ya uzamiaji majini kina kirefu daraja la pili kwa Askari wa Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam. Alipotembelea eneo hilo mapema leo
Mkufunzi kutoka nchini Ujerumani Bw. Dan Jungingfer (kulia), akitoa maelekezo ya mbinu za uzamiaji majini kwenye kina kirefu kwa Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Sajini Gift Longwe na Konstebo Baltazari Swai. Wakati wa  uzinduzi wa mafunzo ya uzamiaji majini kina kirefu daraja la pili kwa Askari wa Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam.
Picha na Jeshi la Zimamoto Na Uokoaji
Na Ripota Wetu,Globu ya Kjamii

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amewasihi viongozi wa dini nchini wasitumie mahubiri yao kuharibu amani au kuleta mgongano katika jamii.

Pia amesema Serikali inatambua wako watu wanaotaka kuharibu amani iliyopo nchini na ametaka watu hao wasipewe nafasi.

Akizungumza katika mkutano mkuu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) uliofanyika Dodoma,Majaliwa amewasihi viongozi wa dini,mahubiri yao yasiwe chanzo cha uvunjifu wa amani na kufafanua Serikali haitasita kuchukua hatua licha ya kwamba inawajali,kuwathamini na kuwaheshimu viongozi wa dini.

Ameeleza kamwe nyumba za ibada zisiwe kiwanda cha kuzalisha chuki.Kuhusu watu wanaotaka kuharibu amani ya nchi,amefafanua Serikali inatambua wapo watu wa aina hiyo.

"Nawaomba viongozi wa dini kutumia Msahafu na Biblia kuhubiri amani," amesisitiza.Kwa upande wa  Waziri wa Nchi ofisi ya Rais Tamisemi Suleiman Jaffo amewaomba viongozi wa dini waendelee kusimamia maadili na amani iliyopo nchini.

Awali Muft sheikh Abubakar Zubeir amesema Bakwata inaendelea na kazi ya kuwaunganisha Waislam wa madhehebu yote.
Mama wa Mtoto Shaibu Alifa akiwa anampeleka mwanae Shule, ambaye anasoma shule ya msingi Mchangani iliyopo wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma. Kampuni ya D and G Export Ltd inayofanya kazi ya kununua korosho katika wilaya ya Tunduru Mkoani Ruvuma imemsaidia baiskeli ya Miguu minne (wheelchair mpya) mtoto Shaibu Alifa mwenye ulemavu wa miguu pamoja tani 3 za saruji kwa ajili ya kukarabati vyoo shuleni ya Mchangani, ujenzi wa zahanati ya Chikomo na kuboresha jengo la tarafa
MKUU wa mkoa wa Tanga, Martine Shigella ametarajiwa kushuhudia mashindano ya riadha ya Tanga City Marathon msimu wa piliyanayotazamiwa kufanyika Jumamosi wiki hii mjini hapa.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mratibu wa Mashindano hayo, Juma Mwajasho alisema maandalizi yamekamilika kwa asilimia kubwa huku baadhi ya washiriki wakithibitisha kushiriki.Alisema katika mashindano hayo msimu huu watazamia washiriki zaidi ya600 ambapo washindi watakabidhiwa zawadi mbalimbali zikiwemo medali ambazo zimeandaliwa na wadhamini wa mashindano hayo.

Aidha alisema mashindano hayo yatashirikisha wakimbaji kwenye umbali wa kilomita 21,10 na 5 ambapo wataanzia mbio hizo kwenye eneo la Mkwabi Super Market kuzunguka maeneo mbalimbali Jijini Tanga na kuishia eneo hilo.“Lakini kwa mara ya kwanza washiriki wote watakaoshiriki mashindano hayo watapewa medali na mgeni rasmi kwenye mashindano hayo.Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Riadhaa Mkoa wa Tanga (RT) Hassan Mwagomba alisema mashindano hayo pia yatashirikisha washiriki kutoka Visiwa vya Shelisheli, Unguja na Pemba ambao watapata fursa yakuonyesha umahiri wao.

Alisema njia zitakazopitia mashindano hayo zimeboreshwa zaidi kiusalama kwa wakimbiaji ili kuweza kuepukana na adhari zinazoweza kujitokeza wakati yakiendelea.Naye kwa upande wake,Meneja wa Mkwabi Super Market ya Jijini Tanga ambao ni waandaaji wakuu wa mbio hizo,Kawkab Hussein alisema msimu huo wameboresha mashindano hayo kwa kutoa zawadi kwa mshindi wa kwanza hadi wa kumi.

Alizitaja zawadi zinazotolewa kuwa ni mshindi wa kwanza km 21 atapata700,000 wa pili 500,000, huku mshindi wa tatu akipata 300,000 huku wengine kuanzia wa nne hadi wa kumi watapata kifuta jasho cha 50,000.

Hata hivyo alisema katika kilomita 10 mshindi wa kwanza atapata 250,000, wa pili 150,000 na wa tatu 100,000 huku washindi wa kuanzia nafasi ya nne mpaka 10 watapewa 30,000 pia kutakuwa na vituo maalumu kwaajili ya kutoa huduma ya maji kwa wakimbiaji (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha).
Mratibu wa Mashindano ya Riadha ya Tanga City Marathon, Juma Mwajasho kulia akitetea jambo na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya kuelekea mashindano hayo Jumamosi wiki hiikushoto ni Meneja wa Mkwabi Super Market ya Jijini Tanga ambao niwaandaaji wakuu wa mbio hizo,Kawkab Hussein na Katibu wa Chama cha Riadha Mkoani Tanga (RT) Hassan Mwagomba
Katibu wa Chama cha Riadhaa Mkoa wa Tanga (RT) Hassan Mwagomba akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na uwepo wawashiriki kutoka Visiwa vya Shelisheli, Unguja na Pemba ambao watapat afursa ya kuonyesha umahiri wao kulia ni Meneja wa Mkwabi Super Marketya Jijini Tanga ambao ni waandaaji wakuu wa mbio hizo,Kawkab Hussein,
Meneja wa Mkwabi Super Market ya Jijini Tanga ambao ni waandaaji wakuu wa mbio hizo, KawkabHussein akizungumza na waandishi wa habari kwenye mkutano huu kuhusiana na zawadi zitakazotolewa msimu huu
Sehemu ya medali zitakazotolewa kwenye mashindano hayo

Tanzania imefanikiwa kuongeza idadi ya watalii kutoka 1,284,279 mwaka 2016 hadi kufikia 1,327,143 mwaka 2017 hali iliyopelekea kuongezeka kwa mapato ya Serikali.

Akizungumza wakati wa Mkutano wa 25 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara ya Maliasili na Utalii uliofanyika mjini Dodoma, Waziri wa Wizara hiyo, Dkt. Hamisi Kigwangalla amesema Wizara yake itaendelea kuvutia watalii wengi zaidi ili kukuza utalii na kuongeza pato la Taifa. 

“Mapato yanayotokana na utalii yameongezeka kutoka Dola za Kimarekani Bilioni 2.1 mwaka 2016 hadi Dola za Kimarekani Bilioni 2.2 mwaka 2017” alisema Dk. Kigwangalla.Akifafanua Dkt. Kigwangala amesema lengo la Serikali ni kuona mafanikio haya yanazidi kuimarika, hivyo kila mtumishi katika Wizara hiyo lazima atimize wajibu wake ipasavyo katika kutimiza lengo la Wizara hiyo ambalo ni kuhifadhi na kusimamia maliasili, malikale na kuendeleza utalii.

Aliongeza kuwa ili kufanikisha majukumu ya Wizara hiyo ipasavyo ni muhimu kuwa na bajeti ambayo itawezesha kushughulikia changamoto za migogoro ya mipaka katika maeneo ya hifadhi, kufanya mapitio ya Sera, Sheria na Kanuni mbalimbali, upungufu wa watumishi, uhaba wa vitendea kazi, kutoa elimu ya maadili na kusimamia watumishi. 

Alisema Wizara yake itaendelea na mapambano dhidi ya ujangili, biashara haramu ya nyara, magogo na kuwachukulia hatua kali za kinidhamu na kisheria kwa watumishi wote watakaogundulika kukiuka maadili ya utumishi wa umma kwa kushiriki katika vitendo hivyo.Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Meja Jenerali Gaudensi Milanzi amesema kuwa Wizara hiyo itazingatia ushauri utakaotolewa na Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo ili kuongeza tija katika kutatua changamoto zinazojitokeza.
Waziri wa Mali Asili na Utalii Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangalla akihutubia Wafanyakazi wa Wizara hiyo wakati wa Mkutano wa 25 wa Baraza la Wafanyakazi wa Wizara hiyo uliofanyika mjini Dodoma jana.
Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Maj. Gen. Gaudensi Milanzi akizungumza na Wafanyakazi wa Wizara hiyo wakati wa mkutano huo.
Baadhi ya wajumbe wa mkutano huo wa baraza wakisikiliza hotuba ya mgeni rasmi, Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla.
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. HamisI KigwangalLa (katikati) akiimba wimbo wa mshikamano pamoja na Katibu Mkuu Wizara hiyo, Maj. Gen. Gaudensi Milanzi pamoja na viongozi wengine wa Shirikisho la Wafanyakazi.
Baadhi ya ya Wakurugenzi na Wakuu wa Taasisi wa Wizara ya Maliasili na Utalii Wakiimba wimbo wa mshikamano wa wafanyakazi wakati wa mkutano huo uliofanyika mjini Dodoma.

Na Mwamvua Mwinyi,Kibaha

KIWANDA cha kutengeneza nguzo za zege cha Hunnan Power ,mjini Kibaha Mkoani Pwani ,kimefungwa kutokana na kukosa tenda na soko , tangu uzalishaji uanze mwezi september mwaka jana.

Kutokana na hali hiyo, kiwanda hicho kimebaki gofu na kupunguza ajira kutoka wafanyakazi 30 hadi wawili kwasasa.Hayo yalibainika wakati wa ziara ya mkuu wa mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo ,alipotembelea viwanda nane vilivyoanza uzalishaji na ambavyo vipo kwenye hatua za ujenzi mjini Kibaha.

Alisema mkoa huo unadhamira ya kuwa ukanda wa Viwanda vinavyozalisha bidhaa mbalimbali lakini endapo soko litakuwa hakuna ,wawekezaji watakata tamaa.Alisema mkoa una viwanda vinavyotengeneza nguzo za zege viwili ikiwemo Hunnan Power /Kibaha na East Africa infrastructure engineering Ltd kilichopo Fukayosi /Bagamoyo ambavyo vinahofiwa kushindwa kuendelea kuzalisha kwasababu ya bidhaa zake kukosa wateja.

"Katika ziara hii tumebaini changamoto ya kiwanda cha Hunnan Power kukosa masoko na tenda huko shirika la umeme (Tanesco ),hawajapata tenda mara tatu ,""Hali hiyo imesababisha kiwanda hicho kufungwa, hakizalishi ,mashine zimefungiwa ndani ,kiwanda kimezungukwa nyasi ,kimekuwa gofu na ajira hakuna" suala hili linaangusha juhudi za rais John Magufuli ,Mkoa na serikali"alisema mhandisi Ndikilo.

Mhandisi Ndikilo alieleza, wawekezaji wanajitoa kuunga mkono na kuitikia wito wa serikali kujenga viwanda lakini baadhi vinakumbana na changamoto ya ukosefu wa soko la uhakika.Aliahidi kuzungumza na waziri mwenye dhamana na mkoa utafuatilia ili waziri wa nishati aweze kusaidia suala hilo.

Mkuu huyo wa mkoa aliitakaTanesco kuangalia kwa jicho la tatu tatizo hilo na kuangalia namna ya kutoa tenda ili kuokoa kuinua viwanda hivyo.Mhandisi Ndikilo alitaja changamoto nyingine alizofikishiwa kwenye ziara hiyo,kuwa ni umeme,maji barabara na vibali kutoka TFDA.Aliwasihi viongozi wa wilaya ,halmashauri kuandika barua moja kwa moja kwa taasisi husika watatue matatizo hayo ili kuwavutia wawekezaji ."Official communication itasaidia kuliko kusumbua sana hawa wawekezaji ,,itakuwa rahisi kufanya ufuatiliaji na kuzibana taasisi husika na kuzisukuma zifanye utekelezaji " alisisitiza.

Awali akitoa taarifa ya kiwanda cha Hunnan Power ,mkalimani wa kiwandani hapo, Suleiman Ramadhani alisema kiwanda kilianza ujenzi Jan 2017 na kuanza uzalishaji September 2017 na kimegharimu dollar milioni mbili na hakijawahi kuuza hata nguzo moja.Alisema kiwanda hakifanyi kazi tangu Jan mwaka huu kwakuwa kinategemea tenda na soko .

Suleiman alielezea kuwa ,wenye viwanda wanahitaji kujenga kiwanda kingine katika eneo hilo lakini wanashindwa kwasasa hadi hapo watakapopata wateja .Mhandisi wa udhibiti wa mapato Tanesco mkoani Pwani ,Fabian Rukiko ,alisema hawajawahi kutumia nguzo za zege mkoani hapo hadi hapo itakapohitajika.

Alikishauri kiwanda hicho kujitangaza kupitia kitengo cha mauzo na masoko kwani itasaidia kufanya ufuatiliaji na kushirikiana na wadau wakubwa watakaoweza kununua bidhaa hiyo muhimu ambayo inadumu kwa kipindi kirefu.Mwezi Novemba 2017, waziri wa Nishati Dk.Merdard Kalemani alitembelea kiwanda cha nguzo za zege kilichopo Fukayosi na alilitaka shirika la umeme Tanesco kutumia nguzo zinazozalishwa nchini kwenye ujenzi wa miradi mikubwa.

Nanukuu":"baada ya serikali kupiga marufuku uingizwaji wa nguzo za umeme toka nchi za nje na kuruhusu wawekezaji kutengeneza nchini, sasa umefika wakati TANESCO ianze kutumia nguzo za zege kuanzia Desemba 2017 kwenye miradi mikubwa";alisema.
Kiwanda cha Hunnan Power kinachotengeneza nguzo za zege mjini Kibaha, kikionekana kutoweza kuendelea na uzalishaji kutokana na kukosa soko na tenda ,na nguzo zikionekana kubaki chini bila mauzo ,wakati mkuu wa mkoa wa Pwani ,Mhandisi Evarist Ndikilo ,alipofanya ziara yake ya siku moja kutembelea viwanda nane mjini hapo.(Picha na Mwamvua Mwinyi)
Mkuu wa mkoa wa Pwani ,Mhandisi Evarist Ndikilo ,alipofanya ziara yake ya siku moja kutembelea viwanda nane mjini Kibaha ambavyo vingine vianza uzalishaji na vingine vikiwa hatua mbalimbali za ujenzi (picha na Mwamvua Mwinyi)
 Askofu Dkt Alex Malasusa wa Kanisa la Kiinjili la Kiluteri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani, (DMP) akisalimiana na Waziri Mkuu wa zamani Mh.Edward Lowassa leo katika ibada ya Ijumaa Kuu
 Askofu Dk Alex Malasusa wa Kanisa la Kiinjili la Kiluteri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Mashariki na Pwani, (DMP) akiomgoza ibada ya   ya i\Ijumaa Kuu leo jijini Dar as Salaam.Picha na Emmanuele Massaka,Globu ya jamii
Waziri Mkuu wa zamani Mh.Edward Lowassa (wa kwanza kushoto) akiwa pamoja na waumini wengine kwenye ibada ya Ijumaa kuu leo jiji Dar as Salaam.

*Awaomba wakazi Jiji la Mwanza kujitokeza kwa wingi,asema ni fursa kwa wanamuziki wa Injili

Na Ripota Wetu,Globu ya jamiii

MBUNGE wa Jimbo la Nyamagana ,Mwanza Stanslaus Mabula ameeleza kufurahishwa ha ujio wa Tamasha la Pasaka 2018 ambalo kwa mara ya kwanza linafanyika Jijini humo.

Ambapo amesema hiyo ni fursa kubwa kwa wasanii wa nyimbo za Injili katika Mkoa huo ambao una vipaji vingi vya waimbaji.

Akizungumza mapema leo na Michuzi Blog jijini Mwanza,Mabula amesema kutokana na ujio wa tamasha hilo, Kwaya nyingi za Jiji la Mwanza zitapata nafasi ya kuonesha uwezo na vipaji vyao vya uimbaji katika suala zima la kumtukuza Mungu kupitia nyimbo za Injili.

“Jiji la Mwanza lina vikundi/kwaya mbalimbali na mahiri katika uimbaji wa nyimbo za injili,hivyo tunaishukuru Kampuni ya Msama Poromotions,kutuletea tamasha la Pasaka litakalofanyika katika uwanja wa CCM Kirumba April Mosi na baadae tamasha hilo litahamia kwa Wakazi wa Mkoa Simiyu ndani ya Mji wa Bariadi Aprili 2,2018,”ameeleza Mabula

Amesema tamasha la Sikukuu ya Pasaka pia litakuwa sehemu ya kuhamasisha utulivu,upendo na amani ya Tanzania ambayo Watanzania wengi wanaihitaji kuiona ikilindwa na kuimarika siku hadi siku.

Ametoa mwito kwa wakazi wa Jiji la Mwanza kujitokeza kwa wingi katika tamasha hilo na kukongwa kwa nyoyo zao kupitia kwa waimbaji mbalimbali akiwemo Rose Muhando ambaye atazindua albamu yake itakayoitwa “USIFE MOYO”.

Wengine ni Upendo Nkone,Bone Mwaitege,Godluck Gozbert,Martha Baraka,Clement Paul,Beatrice Mwaipaja,Christina Shusho,Christopher Mwahangila,Jesca Honole na wengineo.
Mbunge wa Nyamagana,Mh.Stanslaus Mabula akifafanua jambo alipokuwa akizungumzia kuhusu ujio wa Tamasha la Pasaka 2018 kwa mara ya kwanza jijini Mwanza chini ya Kampuni ya Msama Promotions. 
Na Emmanuel Masaka, Globu ya jamii

MAMA mwenye mtoto mwenye nguvu za ajabu anayeishi Mtaa wa Kwa Mbela uliopo Mburahati Mianzini Salama Omar amemuomba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kumsaidia katika matibabu ya mwanaye.

Mbali ya kumuomba Makonda kumsaidia matiabu ya mtoto wake Mzamiry Said(7), pia ametumia nafasi hiyo kuelezea namna ambavyo mumewe aliyefunga naye ndoa mwaka 2009 alivyomtekeleza yeye na mtoto.

Akizungumza na Michuzi blog leo jijini Dar es Salaam Salama amesema anaishi maisha yenye changamoto nyingi anakabiliana nazo katika malezi ya mtoto wake ambaye ameeleza amekwenda kwenye hospitali mbalimbali ikiwemo Hospitali ya Taifa  Muhimbili na CCBRT.

Amefafanua na kote huko alikokwenda madaktari wamechukua vipimo vyote vikiwemo vya kuangalia iwapo ana tatizo la akili au ulemavu lakini wamemthibitisha matatizo hayo ila anakumbuka mmoja wa madaktari wa Muhimbili anayeshughulikia watu wenye magonjwa ya akili anakumbuka alimwambia mwanaye hata pona , hivyo ataendelea kuwa hivyo katika maisha yake yote.

"Ni kweli mwanagu sasa ana maiaka saba na tatizo bado lipo.Ana nguvu nyingi na anapocheza na wenzake unakuwa makini kufuatilia maana anaweza kufanya chochote ambacho si kizuri. Napata shida kwenye malezi ya mwanangu tangu alipozalizwa.

Nimejitahidi katika matibabu lakini hali iko vile vile.Muda wote inabidi niwe namchunga asiende mbali kwani unaweza kumuacha akaenda kucheza na watoto wengine mtaani lakini kutokana na nguvu alizonazo anaweza hata kujeruhi.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Na Leandra Gabriel, Globu ya jamii
MENEJA wa Shirika la Maji safi na maji taka  (DAWASCO) Magomeni Mponjoli Damson ametoa rai kwa wateja wanaounganisha maji kiholela kupitia mita za DAWASCO kuacha mara moja. 

Akizungumza na waandishi wa habari Mponjoli ameeleza kuwa wakazi wa maeneo hayo wamekuwa wakiiba maji kutoka mita za DAWASCO kwa kutokujua au kwa makusudi kabisa kwa maslahi yao binafsi hali inayohatarisha usalama wa mita hizo na kukosa maji wa baadhi ya wakazi wa maeneo hayo.

Amewataka wananchi kutounganisha maji kwa mtu mwingine kupitia mita za mamlaka hizo na kuacha mamlaka husika kufanya kazi yake na kuweza kutoa huduma wa wakazi wote.

Aidha Mponjoli ameeleza kuwa changamoto hii inatokana na wakazi wengi kukosa elimu  kuhusu huduma za kuunganisha maji na kama mamlaka wapo tayari kutoa elimu kwa wananchi wote.

Aidha mponjoli ametoa wito kwa wakazi wa Magomeni kuuliza kwa mamlaka husika kuhusu huduma za kuunganishiwa maji kutoka kwa mamlaka husika sio mteja wa kawaida.

Ameeleza kuwa kama mamlaka wapo tayari kutoa elimu kwa wananchi na kushauri namna ya kuunganisha maji kama inavyostahili sio kiholela.

Mwisho ametoa wito kwa wakazi wa maeneo hayo kufuata sheria na taratibu zilizowekwa na mamlaka hayo na zikikiukwa lazima sheria zifuate mkondo wake kwa kulipa faini na hatua nyingine za kisheria.
Meneja wa Shirika la Maji safi na maji taka (DAWASCO) Magomeni, Mponjoli Damson akionesha moja ya pampu za maji walizozikamata kwa wateja waliounganisha maji kiholela kupitia mita za DAWASCO

Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

SWALI ambalo mashabiki wa msanii na mwigizaji wa filamu nchini Snura Mushi kama atatoa wimbo mpya au filamu ,jibu swali kupatikana Aprili mwaka huu.

Kwa muda mrefu mashabiki wa muziki na Watanzania wamekuwa wakiuliza kupitia mitandano ya kijamii ni lini Snura atavunja ukimya kwa kuja na kituo.

Akizungumza leo Dar es Salaam,Menaja wa Snura,anayejulikana kwa jina la Hemed Kavu a.k.a amesema swali hilo ni fumbo kubwa.

Hata hivyo amesema Aprili mwaka huu Snura atakuja na ujio mpya katika medani ya muziki pendwa wa Bongo Fleva.
"Matarajio yetu ni kwamba Snura Aprili mwaka huu atavunja ukimya kwa kuweka wazi kuhusu swali hill lenye hastah ya Vumbi LA mguu," amesema HK.
Uwezo,kipaji, kukata nyonga,sauti na mvuto wa Snura umemfanya kuwa na umaaarufu wake katika medani ya muziki wa kizazi kipya na filamu za kibongo kwa ujumla.
"Matarajio yetu ni kwamba Snura Aprili mwaka huu atavunja ukimya kwa kuweka wazi kuhusu swali hill lenye hastah ya Vumbi LA mguu," amesema HK.
Hivyo kwa sasa mashabiki wanasubiri kwa hamu kubwa kuona nini ambacho mwanamuziki huyo amekiandaa kwa ajili yao maana hajawahi kukosea.
"Matarajio yetu ni kwamba Snura Aprili mwaka huu atavunja ukimya kwa kuweka wazi kuhusu swali hill lenye hastah ya Vumbi LA mguu," amesema HK.

Na Genofeva Matemu – WHUSM
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amemtaka Msanii wa muziki wa bongo fleva Roma Mkatoliki kujisajili BASATA ili aweze kuondolewa kwenye kifungo chake cha kutokufanya shughuli za sanaa kwa miezi sita alichofungiwa mwanzoni mwa mwezi machi mwaka huu.
Hayo ameyasema wakati wa kikao na waandishi wa habari jana Jijini Dar es Salaam baada ya kikao na wasanii wa mziki Roma Mkatoliki na Pretty Kind ambapo Wizara ilimtaka msanii Roma kubadilisha wimbo wake wa kibamia na kujisajili BASATA ili aweze kuondolewa katika kifungo hicho ambapo msanii huyo alitangaza kuufuta wimbo huo na kuahidi kujisajili BASATA ili aweze kuendelea na mziki.
“Kwa kuwa msanii Roma Mkatoliki ameamua kuufuta kabisa wimbo wa kibamia na kuvitaka vyombo vya habari kutokuucheza tena wimbo huo Wizara inamfungulia kifungo chake mara tu baada ya kujisajili BASATA atakuwa huru kuendelea na kazi zake za sanaa” amesema Mhe. Mwakyembe
Aidha Naibu Waziri Shonza amesema kuwa Msanii Suzan Michael (Pretty Kind) ametambua kosa alilolifanya na kukiri kosa hilo kwa kufanya jitihada mbalimbali ikiwemo kuandika barua ya kuomba msamaa na kujisajili BASATA kuwa msanii halali hivyo Wizara kwa kushirikiana na BASATA imeridhia kumfungulia adhabu aliyopewa ya miezi sita ambayo kimsingi ilitakiwa kuisha tarehe moja julai mwaka huu. 
“Kuanzia sasa msanii Pretty Kind yupo huru kuendelea na kazi zake za sanaa kutokana na yeye kutimiza matakwa aliyoagizwa kuyafanya na kuahidi kuwa balozi mwema wa masuala ya maadili kwa wasanii wenzake” amesema Mhe. Shonza.
 Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) baada ya kufanya kikao na wasanii wa mziki Roma Mkatoliki na Pretty Kind jana jijini Dar es Salaam. Pembeni kwa waziri ni Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza
 Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kulia) akifafanua jambo wakati wa kikao na waandishi wa habari baada ya kufanya mazungumzo na wasanii Roma Mkatoliki na Pretty Kind jana Jijini Dar es Salaam. Katikati ni mwakilishi kutoka Bodi ya Filamu Bw. Benson Mkenda na kushoto ni msanii wa mziki Pretty Kind
 Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kushoto) akiwaonyesha waandishi wa habari nakala ya cheti cha usajili cha msanii Pretty Kind kutoka BaASATA wakati wa kikao na waandishi wa habari jana Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe
 Msanii wa mziki wa bongo fleva Roma Mkatoliki (kulia) akizungumza na waandishi wa habari jana Jijini Dar es Salaam baada ya kufanya kikao na Waziri pamoja na Naibu Waziri ambapo alitangaza kuufuta na kuviomba vyombo vya habari kutoucheza tena wimbo wake wa kibamia. Kushoto ni Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe katika picha ya pamoja na Msanii Roma Mkatoliki (wapili kushoto) na msanii Pretty Kind (kulia) baada ya kuzungumza nao na kurekebisha tofauti zilizopelekea kufungiwa kwa wasanii hao jana Jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza 
Picha na: Genofeva Matemu - WHUSM

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

*Kamanda Mambosasa agusia upelelezi kifo cha Akwilina 

Na Leandra Gabriel, Globu ya jamii

KAMANDA wa Kanda Maalumu ya Dar es salaam Lazaro Mambosasa amesema  hali ya usalama wa Jiji kuelekea Sikukuu ya Pasaka na wamejiimarisha kulinda usalama wa raia na Mali zao.

Mambosasa ameeleza kuwa Jeshi limejipanga kwa kuimarisha ulinzi na kuhakikisha wakazi wa jiji la Dar es salaam wanasherekea vizuri sikukuu hii.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam,Mambosasa ameeleza hakuna mtu yeyote atakayepata fursa ya kufanya tukio lolote la kiharifu kwani jeshi limejipanga kwa doria ya miguu, mbwa, pikipiki, farasi na magari yote yaliyopo katika kuhakikisha usalama wa raia wote na pia wameongeza nguvu ya ulinzi katika fukwe zote.

Kuhusu disko toto Mambosasa amesema kuwa hakuna kibali kilichoombwa hivyo hategemei kuona kumbi yoyote itakayokusanya watoto.

Kuhusu mauaji ya Akwilina Akwilini kamanda Mambosasa ameeleza upelelezi bado unaendelea na maelezo waliyoyapata bado wanayafanyia kazi uchunguzi ukikamilika watatoa maelezo.

Ametoa rai kwa waendesha vyombo vya moto kuwa makini na kuepukana na ulevi ili kulinda usalama wao na wananchi kwa ujumla.