Benki ya Maendeleo ya Kilimo nchini (TADB) imeazimisha Siku ya Wanawake Duniani kwa kuendesha mafunzo ya kilimo kwa wanawake wakulima wa Chama cha Ushirika Ruvu (CHAURU) ili kuwajengea uwezo ili Kuchagiza na kusaidia Mapinduzi ya Kilimo kutoka kilimo cha kujikimu kwenda cha kibiashara ili kuchangia kwenye ukuaji wa uchumi na kupunguza umaskini.

Akizungumza na wanawake hao, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TADB, Bibi Rosebud Kurwijila alisema kuwa moja ya malengo ya kimkakati ya TADB ni kuhamasisha kilimo cha kisasa na cha kibiashara kwa wakulima wadogo wadogo hasa wanawake na vijana nchini.

Aliongeza kuwa Benki ya Kilimo ina mikakati ya dhati katika kuwasaidia wakulima wanawake nchini ili hasa katika kutekeleza kwa vitendo Kauli mbiu ya kitaifa ya Siku ya Wanawake Duniani Mwaka huu 2018 isemayo ”Kuelekea uchumi wa viwanda tuimarishe usawa wa jinsia na uwezeshaji wa wanawake vijijini.’’ 

“Katika hili TADB inatambua mchango wa wanawake katika sekta ya kilimo ambao wengi wao wako vijijini na ndio wazalishaji wakubwa wa chakula katika taifa letu,” alisema.  
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TADB, Rosebud Kurwijila akizungumza na wanawake wanaojishughurisha kilimo walio chini ya mwavuli wa CHAURU na Faraja Women’s Group (hawapo pichani).
 Afisa Biashara Mwandamizi wa TADB, Eunice Mbando akizungumza na wanawake kuhusu fursa za mikopo nafuu kwa wakulima itolewayo na Benki ya Kilimo nchini.
 Baadhi ya wanawake wanaojishughurisha kilimo walio chini ya mwavuli wa CHAURU na Faraja Women’s Group  wakifuatilia kwa makini mafunzo yaliyotolewa na Benki ya Kilimo nchini.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...