Maofisa wa kampuni ya Coca-Cola mkoani Mwanza, kutoka kushoto Meneja Mauzo Mkoa , Mnyamuhanga Gavana,Meneja Mauzo na Masoko Samuel Makenge na Meneja Mauzo Mwandamizi Deus Kadico, wakionyesha mfano wa chupa zenye vizibo vyenye zawadi ya promosheni ya ‘Mzuka wa Soka na CoKa’ iliyozunduliwa jijini humo.
Meneja Mauzo na Masoko wa kampuni ya soda ya Cocacola tawi la Mwanza Samuel Makenge, akizungumza na waandishi wa habari jijini Mwanza wakati wa uzinduzi wa promosheni. 

 Lengo ni kuwezesha wapenzi wa soka kupata burudani ya Kombe la Dunia 2018 Wakati michuano ya Kombe la Dunia 2018, ambayo mdhamini wake mkuu ni kampuni ya Coca-Cola inakaribia kuanza,kampuni ya kutengeneza vinywaji ya Nyanza Bottlers leo imezindua promosheni itakayotoa fursa kwa wateja wake kujishindia luninga za kisasa, zitakazowezesha kufaidi uhondo wa michuano ya kombe la dunia wakiwa majumbani kwao. 

 Promosheni hii ambayo inajulikana kama ‘ Mzuka wa Soka na CoKa’ itawahusu watumiaji wa soda za Coca-Cola, Sprite, Fanta, Sparleta na Stoney Tangawizi katika mikoa ya Kanda ya ziwa . Mbali na zawadi za televisheni,watumiaji wa vinywaji vya kampuni ya Coca-Cola, kupitia promoheni hii wataweza kujishindia zawadi nyinginezo mbalimbali ikiwemo ,fedha taslimu kati ya shilingi 5,000 mpaka shilingi 100,000/-kofia, t shirt,soda za bure na zawadi kubwa ya bodaboda. 
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...