MKUU wa Wilaya ya Kibaha Bi Assumpter Mshama amewaahidi kina mama wajasiriamali wa Wilaya ya Kibaha kuwa atazungumza na uongozi wa Halmashauri ya Mji  ili itengwe  siku na eneo maalum  kwa ajili ya kufanya maonyesho  ya bidhaa wanazozitengeneza ikiwa ni katika kupambana na  changamoto ya ukosefu wa masoko ya kuuzia bidhaa hizo.
Mshama amesema hayo alipokuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya wanawake  duniani  Kibaha Mkoa wa Pwani, amewataka wanawake kujiamini, kushikamana  na kuachana na dhana potofu ya kupigana vita katika maeneo mbalimbali kwani adui wa mwanamke ni mwanamke mwenyewe.
Aidha amesema  kutokana na wanawake wengi  kutofahamu  sheria za ndoa na mirathi , talaka  na sheria ya ardhi  ya mwaka 1999, Halmashauri ya Kibaha  itaendelea kutoka elimu  ya sheria kwa kupitia wadau wa masuala  ya sheria.
Amewataka wanawake wote nchini kuitafakari siku hii maalum  kwa kutafakari mafanikio na changamoto na kuweka  utatuzi wa changamoto wanazokabiliana  nazo wanawake huku  kauli mbiu  ikisema  kuelekea uchumi wa viwanda tuimarishe uswa wa jinsia  na uwezeshaji wanawake vijijini kauli mbiu hii inahamasisha  jamii kuongeza fursa za kiuchumi  kwa wanawake  ili kuwajengea uwezo  katika nyanja zote  za maendeleo, kiuchumi, kisiasa, kiutamaduni na kitaaluma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...