-Draw ya mechi za Play-Off za Caf Confederation Cup kufanyika leo makao makuu ya CAF, Cairo Misri majira ya Saa 8:30 Mchana

-Draw hiyo inahusisha timu 32 timu 16 ambazo zilitolewa kwenye klabu bingwa Afrika (Caf Champions Leagu) na timu 16 ambazo zilifuzu hatua ya 16 bora kutoka kombe la Shirikisho (Caf Confederation Cup)

-Kutakuwa na Pot 4, ya Kwanza ni Pot A itakuwa na timu 4 ambazo zipo juu kwenye Rank ya klabu  kwa timu zilizotolewa kwenye Caf Champions League timu hizo ni Al hilal Omdurman (Sudan), St George (Ethiopia), As Vita Club (DR Congo) na Zanaco (Zambia).

-Pot ya Pili ni Pot B ambayo itakuwa na timu 4 ambazo zina Rank kubwa kwa vilabu kutoka kwenye timu 16 ambazo zilifuzu 16 bora ya Caf Confederation Cup timu hizo ni USM  Alger (Algeria), Super Sport United (Afrika kusini), Hilal Obayed (Sudan) na Enyimba (Nigeria).

-Pot ya Tatu ni Pot C ambayo itakuwa na vilabu 12 ambavyo vimebaki zilizotolewa kwenye Caf Champions League Timu hizo ni UD Songo (Msumbiji), Yanga Sc (Tanzania), CF Mounana (Gabon), Bidvest Wits (Afrika Kusini), Williamsville AC (Ivory Coast), Génération Foot (Senegal), Mountain On Fire (Nigeria), Plateau United (Nigeria), Gor Mahia (Kenya), Asec Mimosas (Ivory Coast), Rayon Sports (Rwanda) na Aduana Stars (Ghana).

-Na Pot ya 4 itakuwa Pot D ambayo itakuwa timu 12 ambazo zimebaki baada ya kutoa 4 (16-4=12) ambazo zilifuzu kutoka Caf Confederation Cup timu hizo ni La Mancha (Congo Brazzavile), Belouizdad  (Algeria), Djoliba (Mali), RSB Berkane (Morroco), Raja Casablanca (Morocco), Al Masry (Misri), Fosa Juniors (Madagascar), CARA Brazzavile (Congo Brazzaville), Costa do Sol (Msumbiji), Akwa United (Nigeria), Deportivo Niefang (Equatorial Guinea) na Welayta Dicha (Ethiopia)

-Wataanza draw na Pot A  vs Pot C kwa timu 4 kutoka Pot A na Timu 4 kutoka Pot C. wanaenda Pot B vs Pot D kwa timu 4 kutoka Pot B na Timu 4 kutoka Pot D baada ya hapo zitakuwa zimebaki timu 8 kutoka Pot C na Timu 8 kutoka Pot D wanachezesha tena Pot C vs Pot D kwa timu 8 kutoka Pot C na Timu 8 kutoka Pot D hapa maana yake ni kwamba timu ambazo zipo Pot A na Pot B haziwezi kukutana  kutokana na kuwa na ranking kubwa Afrika kwa miaka 5 iliyopita.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...