Na Leandra Gabriel,Globu ya jamii
FARU dume mweupe maarufu kama Sudan amefariki akiwa na umri wa miaka 45.

Imeelezwa kuwa kifo chake kilisababishwa na matatizo ya kiafya hasa umri wake ambapo ilisababisha kudhoofu.Hadi kifo kinamkuta Sudan alikuwa chini ya ulinzi mkali dhidi wa majangili.

Jumanne wiki iliyopita ilitangazwa kuwa hali ya Sudan sio nzuri na amekuwa chini ya uangalizi  maalumu katika hifadhi ya Ol Pejeta nchini Kenya.

Aidha Mwakilishi wa hifadhi ya Ol Pejeta Sampere Elodie amemuelezea Sudan kama Faru jasiri aliyekuwa mlinzi wa wenzake dhidi ya majangili mbugani hapo na aliogopwa kutokana na umbo na muonekano wake.

Aidha imeelezwa baadhi ya jeni (genetics) zake zimeweza kuhifadhiwa na zawezwa kupandikizwa kwa  mmoja wa faru aliowaacha (Najin) kupitia seli ili kuweza kupata faru wa aina yake tena.

Faru Sudan ameacha faru jike wawili wa aina yake (mtoto na mjukuu) maarufu kama Najin na Fatu ambaye ni tasa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...