NA TIGANYA VINCENT

19 MACHI 2018

SERIKALI ya Mkoa wa Tabora kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa huo imeamua kumsimamisha Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Kitete Dkt. Nassoro Kaponta ili kupisha uchunguzi wa tuhuma zilizotolewa na wananchi dhidi ya Hospitali hiyo.

Maazimio hayo yalitolewa jana mjini hapa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri mara baada ya kikao na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na Wafanyakazi wa Hospitali ya Mkoa Kitete.

Alisema Dkt Kaponta anasimamisha sio kama yeye katenda kosa bali ni katika uwajibikaji ili kupitisha Kamati Maalumu ya Kuchunguza Kitaalamu (Therapeautic Committee) kwa ajili ya kufanyia uchunguzi wa tuhuma zilizotolewa na wananchi kuhusu mwenendo wa wa Watumishi wa Hospitali hiyo ambaye yeye alikuwa akiisimamia.

Mwanri alitaja baadhi ya tuhuma ni pamoja na lugha chafu kutoka kwa baadhi ya Wauuguzi wanazitoa kwa wakimama wajawazito wanapokwenda kupatiwa huduma ya kujifungua, wagonjwa kudaiwa rushwa na baadhi ya wafanyakazi na vifo wa wakinamama vinavyotokana na uzembe.

Alisema pamoja na Kamati hiyo kuchunguza mambo ya Kitaaluma pia Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB) Mkoani Tabora imepewa jukumu la kuchunguza tuhuma zinazotolewa na wananchi wanaoenda kutibiwa pale za rushwa na lugha chafu.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...