Kamati ya Kudumu ya Bunge Biashara na Mazingira mwishoni mwa wiki imetembea chanzo cha Maji
‘Mkaa’ kilichopo Tarafa ya Kiponzelo, Kata ya Ifunda, Mkoani Iringa.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Innocent Bashungwa ameupongeza uongozi wa Mkoa
wa Iringa kwa jitihada zao za kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya kunyweshea mifugo ili
kuendelea kulinda vyanzo vya maji na kuwataka kuondoa miti iliyopo pembezoni mwa chanzo
hicho ambayo inanyonya maji kwa wingi.
Kwa upande mwingine, Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe.
Kangi Lugola amezitaka Halmashauri na Wilaya zote nchini kupanda miti kwa wingi ambayo ni
rafiki kwa mazingira. “Endapo tutapanda miti kwa wingi, tutaendelea kuwa na mvua za kutosha
na kila Halmshauri zinatakiwa kuwa na Sheria ndogo ndogo za Mazingira”.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza amewataka waheshiwa wabunge kuwa mstari wa
mbele kuhimiza kilimo cha umwagiliaji kwa kutimia ‘matone’ ili kupunguza matumizi ya maji
katika maeneo yao.
Diwani wa Kata ya Ifunda Bw. Elicus Chumila Ngwetta akifafanua jambo mbele ya Kamati ya
Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira mara baada ya kutembelea eneo la
Ifunda na kujionea chanzo cha maji ‘Mkaa’ kilichohifadhiwa vizuri. Uhifadhi wa vyanzo vya maji
ni muhimu sana kwa mustakabali wa nchi yetu. Kulia ni Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais
(Muungano na Mazingira) Mhe. Kangi Lugola.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Kangi Lugola akifafanua jambo mbele ya Kamati ya
kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira. Kamati ya Bunge mwishoni mwa wiki
ilipata fursa ya kutembelea chanzo cha maji ‘Mkaa’ kilichopo Tarafa ya Kiponzelo, Kata ya
Ifunda, Mkoa wa Iringa.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Kangi Lugola akisisitiza jambo mbele ya Kamati ya
kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira mara baada ya kutembelea chanzo cha
maji ‘Mkaa’ kinachopeleka maji yake Mto Lyandembela ambao nao unamwaga maji Ruaha
Mkuu mwaka mzima, Mto ambao ni muhimu sana kwa ustawi wa viumbe hai. Kushoto ni Mhe.
Hawa Mwaifunga na kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Innocent Bashungwa.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi. Amina Masenza akiwaonyesha waheshimiwa wabunge wa Kamati
ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira eneo maalumu lililotengwa kwa ajili ya mifugo
kunywa maji katika eneo la Ifunda ikiwa ni jitahada za Mkoa huo kuhifadhi vyanzo vya maji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...