KAMATI ya kitaifa inayoendesha mradi wa pamoja kati ya mashirika matatu ya Umoja wa Mataifa (UNESCO, UN Women na UNFPA) na serikali ya Tanzania kupitia wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na wizara nyingine ambazo zinahusika na maswala ya Elimu hususani TAMISEMI, Wizara ya Afya, Maedeleo ya Jamii, Jinsia, Watu Wazima na Watoto na Wizara ya Sheria na Katiba pamoja na mfadhili wa mradi KOICA imekutana kwa mara yake ya kwanza kujadili mwelekeo wa mradi unawo husu kumwendeleza msichana na mwanamke kijana kupitia elimu.
Mkutano huo uliokuwa chini ya Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk Leonard Akwilapo uliangalia na kubadilishana mawazo ya hatua zilizofikiwa katika mradi huo ulioanza mwaka 2016 na kutekelezwa katika wilaya nne nchini Tanzania (Kasulu, Ngorongoro, Sengerema na Mkoani, Pemba) kwenye kata 22 na kupitia mpango wa mwaka 2018.
Akizungumza kabla ya kusimamia mazungumzo, Dk Akwilapo aliwashukuru wafadhili na pia wadau wengine waliojipanga kufanikisha mradi huo muhimu kwa maendeleo ya wanawake nchini Tanzania na uchumi kwa ujumla.
“Mradi huu ni muhimu sana kwetu, kwa kuwa unachangia juhudi za Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (MoEST) na wizara nyingine zinazofanyakazi kwa pamoja bila kuchoka kuchangia maendeleo ya sekta ya elimu zikiwemo Wizara za Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu na Wizara ya Katiba na Sheria MoCLA” alisema.
Mgeni
rasmi Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk Leonard
Akwilapo akitoa hotuba ya ufunguzi wa mkutano wa Kamati ya Kitaifa ya UN
na Serikali ya mradi wa unaofadhiliwa na KOICA wa kuendeleza wasichana
na wanawake vijana kielimu uliofanyika katika Hoteli ya Protea Courtyard
jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mkazi wa KOICA nchini, Joonsung Park ambao ndio wafadhili wa mradi huo
akizungumza wakati wa mkutano wa Kamati ya Kitaifa ya UN na Serikali ya
mradi wa unaofadhiliwa na KOICA wa kuendeleza wasichana na wanawake
vijana kielimu uliofanyika katika Hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar
es Salaam.
Mwakilishi
wa Mkurugenzi wa UNESCO Kanda ya Afrika Mashariki, Viola Kuhaisa
akizungumza kwa niaba ya Anne Theresa Ndog-Jatta wakati wa mkutano wa
Kamati ya Kitaifa ya UN na Serikali ya mradi wa unaofadhiliwa na KOICA
wa kuendeleza wasichana na wanawake vijana kielimu uliofanyika katika
Hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi
wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Wanawake (UN Women) Hodan Addou
akitoa salamu za UN WOMEN katika kufanikisha utekelezaji wa mradi huo
kwa mwaka 2018 unaohusu kumwendeleza msichana na mwanamke kijana kupitia
elimu unaofadhiliwa na KOICA uliofanyika katika Hoteli ya Protea
Courtyard jijini Dar es Salaam
Kaimu
Mkuu wa Ofisi za Unesco nchini, Faith Shayo akizungumza jambo kabla ya
kumkaribisha mwakilishi wa Mkurugenzi wa UNESCO Kanda ya Afrika
Mashariki, Viola Kubaisa (hayupo pichani) wakati wa mkutano wa Kamati ya
Kitaifa ya UN na Serikali ya mradi wa unaofadhiliwa na KOICA wa
kuendeleza wasichana na wanawake vijana kielimu uliofanyika katika
Hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam. Mgeni rasmi Katibu Mkuu
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk Leonard Akwilapo (katikati)
na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Wanawake (UN Women)
Hodan Addou (kushoto).
Ofisa
Mradi wa Shirika la Sayansi, Elimu na Utamaduni la Umoja wa Mataifa
(UNESCO) nchini, Jennifer Kotta akiwasilisha mada kuhusu utekelezaji wa
mradi kwa mwaka 2018 wakati wa mkutano wa Kamati ya Kitaifa ya UN na
Serikali ya mradi wa unaofadhiliwa na KOICA wa kuendeleza wasichana na
wanawake vijana kielimu uliofanyika katika Hoteli ya Protea Courtyard
jijini Dar es Salaam.
Afisa
Programu anayeshughulikia masuala ya Afya ya Uzazi wa Shirika la Umoja
wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA), Fatina Kiluvia akishiriki katika
mkutano wa kujadili utekelezaji wa mradi kwa mwaka 2018 unaohusu
kumwendeleza msichana na mwanamke kijana kupitia elimu unaofadhiliwa na
KOICA ambao umefanyika katika Hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es
Salaam
Mgeni
rasmi Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk Leonard
Akwilapo katika picha ya pamoja na washiriki wa mkutano wa Kamati ya
Kitaifa ya UN na Serikali ya mradi wa unaofadhiliwa na KOICA wa
kuendeleza wasichana na wanawake vijana kielimu uliofanyika katika
Hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...