Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan jana aliwezesha kupatikana kwa shilingi bilioni moja na milioni mia saba kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Muheza.

Katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye hotel ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam, Makamu wa Rais aliwapongeza uongozi wa Wilaya ya Muheza na mkoa wa Tanga pamoja na wananchi kwa kuamua kujenga hospitali yao ya wilaya ili kuboresha hali ya Afya na Ustawi wa Jamii.

Makamu wa Rais alisema Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuimarisha ubora wa huduma za afya ikiwa ni pamoja na kupunguza idadi ya vifo vya watoto kutoka kiwango cha vifo 66 kati ya vizazi hai 1,000 hadi kufikia kiwango cha angalau vifo 40 kati ya vizazi hai 1,000. Aidha, Serikali imedhamiria kupunguza vifo vya wanawake wajawazito kutoka 556 kwa mwaka 2017 katika vizazi hai 100,000 hadi kufikia 292 ifikapo mwaka 2020.

Sambamba na hilo Serikali kwa kushirikiana na Wadau wa Maendeleo tuna mkakati wa kujenga, kukarabati na kupanua miundombinu ya Vituo vya afya 208 ili kuimarisha utolewaji wa huduma mbalimbali za afya.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa hafla ya uchangiaji wa ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Muheza iliyofanyika jana usiku katika hotel ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akizungumza  wakati wa hafla ya uchangiaji wa ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Muheza iliyofanyika jana usiku katika hotel ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
  aziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Seleman Jafo akizungumza wakati wa hafla ya uchangiaji wa ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Muheza iliyofanyika jana usiku katika hotel ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
  Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigela akizungumza wakati wa hafla ya uchangiaji wa ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Muheza iliyofanyika jana usiku katika hotel ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza wakati wa hafla ya uchangiaji wa ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Muheza iliyofanyika jana usiku katika hotel ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Martine Shigela(kushoto) akimkabidhi Makamu wa Rais zawadi mara baada ya kumalizika kwa zoezi la uchangiaji jana kwenye hotel ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam​

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...