Mkazi wa Moshi Ndugu Erasto Dismas Floridi (22) akabidhiwa bajaji yake mara baada ya kuibuku kuwa mmoja kati ya washindi wa promosheni ijulikanayo kama Jiongeze na Mpesa, Shinda na SportPesa inayoendesha na kampuni ya michezo ya mubashiri SportPesa wakishirikiana na kampuni ya mtandao wa simu za mkononi Vodacom PLC.

Najishughulisha na biashara ya duka kama unavyoona na watu wa kwanza juwapa taarifa juu ya ushindi wangu ni marafiki zangu, kusema ukweli hakuna aliyeamini juu ya ushindi wangu mimi mwenyewe sikuamini ila nikasema ngoja nione mwisho wa hichi kitu utakuwaje”

Sikuwahi kufikiria kama siku ntapata bajaji katika maisha yangu, hii ni zawadi kubwa kwangu na naimani itabadili maisha yangu kwa kiasi kikubwa kwa sababu ntaifanyia biashara na pesa ntakayoipata ntawekeza ili kuchukua mkopo na kufungua duka langu mwenyewe huku biashara yangu ikiwa inaendelea”
Mimi ni kaka wa familia na nina mdogo wangu ambaye namsomesha kwa sababu mama yetu ni mjane kupitia bajaji hii itakuwa imetusaidia sana kwenye kulipia vitu mbali mbali vya familia ikiwemo kumalizia nyumba yetu”.

Kwa upande wa SportPesa Meneja Uhusiano Bi. Sabrina Msuya alisema “Mpaka sasa mkoa wa Mwanza unaongoza kwa kupata washindi watatu huku mikoa mingine kama Dar es Salaam, Mbeya, Kilimanjaro, Nj’ombe, Mara, Musoma Songea na Sumbawanga ikiwa na mshindi mmoja mmoja”

“Pointi zetu za kuweka ubashiri wako ni nzuri kulinganisha na kampuni nyingine, endapo mteja wetu atashinda kwenye ubashiri wake pesa itaingizwa muda huo huo mara baada ya mechi kuisha, kitengo chetu cha huduma kwa wateja kinafanya kazi saa ishirini na siku saba za wiki ili kuhakikisha mteja wetu anapata huduma inayostahili sambamba na kuhakikisha inasikiliza na kutatua matatizo ya wateja wetu.”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...