MASHIRIKA yasiyo ya Kiserikali nchini (NGOs) yaaswa kuwasilisha taarifa za Mwaka kwa mujibu wa Kifungu Na. 29 cha Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 24 ya mwaka 2002 na Kanuni Na. 10 ya Kanuni za Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya mwaka 2004 (GN 152, 2004) kabla ya tarehe 15 Aprili, 2018.

Hayo yameainishwa katika taarifa ya Msajili wa Mashirika yasiyo ya kiserikali Marcel Katemba kwa vyombo vya habari  jijini Dar es Salaam leo. Taarifa hiyo inaeleza kuwa “Mashirika yasiyo ya kiserikali kuwasilisha Taarifa za Mwaka kwa mujibu wa Kifungu Na. 29 cha Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Na. 24 ya mwaka 2002 na Kanuni Na. 10 ya Kanuni za Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya mwaka 2004 (GN 152, 2004), kama ilivyorekebishwa na Kanuni Na. 6 ya Kanuni za Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya mwaka 2014 (GN 8, 2015)”.

 “Taarifa hiyo ijumuishe Taarifa za utendaji kazi, Taarifa za fedha zilizokaguliwa, NGO Fomu Na.10 na Stakabadhi ya malipo ya ada ya mwaka” 

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Mashirika yatakayoshindwa kutekeleza agizo hili ndani ya kipindi tajwa, yatachukuliwa hatua stahiki ikiwa ni pamoja na kutozwa faini. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...