Mvua kubwa iliyonyesha usiku wa kuamkia leo katika eneo la Nyahua wilayani Uyui Mkoani Tabora imesababisha kukatika kwa barabara kuu ya Tabora kupitia Itigi hadi Dodoma na kusababisha magari ya abiria na mizigo kwishindwa kuendelea na safari zake kwa kutumia barabara hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana katika eneo la tukio Meneja wa Wakala wa Barabara )TANROADS) Mkoa wa Tabora Mhandisi Damian Ndabalinze alisema mvua zilizonyesha katika maeneo hayo zimesababisha kukatika kwa eneo hilo ambapo ndipo barabara ya lami inaishia.
Aliwataka madereva wa magari ya aina yoyote kudiriki kupita katika aina hilo kwa sababu wanaweza kuhatarisha maisha yao na abiria na mizigo.
Ndabalinze alisema dereva yoyote atakayekaidi na kuamua kupita katika eneo hilo kwa kulazimisha jambo lolote litakalompata itakuwa ni yeye kajisababishia na asilelekeze lawama kwa chombo chochote.
Baadhi ya wasafiri na wakazi wa Nyahua wilayani Uyui wakiwa katika eneo
ambalo barabara imekatika kutoka na mvua zinazoendelea kunyesha na
kusababisha kukatika kwa mawasiliano baina ya Itigi na Tabora. Nyuma ni
basi dogo la Prince Ramigo linalofanya safari zake kutoka Tabora kwenda
Dodoma kupitia Itigi.
Baadhi
ya wasafiri kutoka katika Basi la Prince Ramigo na wakazi wa Nyahua
wilayani Uyui wakijaribu kuvuka jana katika eneo ambalo barabara
imekatika kutoka na mvua zinazoendelea kunyesha na kusababisha kukatika
kwa mawasiliano baina ya Itigi na Tabora. Nyuma ni basi dogo la Prince
Ramigo linalofanya safari zake kutoka Tabora kwenda Dodoma kupitia
Itigi.
Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa wa Tabora, Mhandisi
Damian Ndabalinze akizungumza na waandishi wa habari na wasafiri jana
mara baada ya kutembelea eneo la tukio ili kujionea uharibifu wa
barabara ulitokana na mvua kubwa iliyonyesha na kusababisha kukatika kwa
mawasiliano baina ya Itigi na Tabora
Kamanda
wa Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoani Tabora SP Emilian Kamuhanda
akizungumza na waandishi wa habari na wasafiri jana mara baada ya
kutembelea eneo la tukio ili kujionea uharibifu wa barabara ulitokana na
mvua kubwa iliyonyesha na kusababisha kukatika kwa mawasiliano baina ya
Itigi na Tabora na kisha kutoa tahadhari kwa Madereva kutodiriki kupita
katika eneo hilo.
Basi la Prince Ramigo linalosafirisha abiria kutoka Dodoma kwenda
Tabora likiwa limekwamwa katikati ya maji jana mara baada ya Dereva
kujaribu kupita. Picha na Tiganya Vincent
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...