• Maaskofu waukana Ujumbe wa Pasaka.
• Maaskofu 4 wa TEC waliouandika wajulikana
Majina yao haya hapa, kwa taarifa za uhakika.
Nimeshtushwa sana na taarifa niliyoipata juu ya Ujumbe wa Kwaresima uliotolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) ulioelekezwa kwa waumini wakati huu wa toba ya Kwaresima iliyoanza Februari 14, 2018 hadi Pasaka siku ya kusherehekea ufufuko wa Bwana Yesu Kristo (Pasaka).

Mimi ni Mkatoliki wa Jimbo la Dodoma na Askofu wangu ni Mhashamu Askofu Mkuu Beatus Kinyaiya.
Nikiri nilianza kupata mashaka tangu mapema ujumbe huu ulipotoka, nilijiuliza sana na hivyo nikaamua kufanya juhudi za kujua kama kweli Kanisa langu Katoliki limefikia hatua hii? Naujua utaratibu na utamaduni wa kanisa langu ndio maana nilipatwa na mashaka haya.

Kwa ambao hawajausoma ujumbe huu, ulikuwa na sura nne lakini iliyoleta tafrani ni sura ya tatu yenye ujumbe kuhusu “Dalili za nyakati zetu Tanzania” hususani katika kipengele cha siasa. Imeleta tafrani kwa sababu katika eneo hili ujumbe huu umeenda kwenye masuala ambayo siku zote yamesababisha kuwepo malumbano kuwa viongozi wa dini wanaingia mambo ya kisiasa ama wanachanganya dini na siasa.

Kwa ufupi kabisa ujumbe huu umetoa shutuma na bila shaka dhidi ya Serikali inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli kuwa shughuli za siasa kama vile uenezi, mikutano ya hadhara, maandamano, makongamano, mijadala na mikutano ya ndani zinazuiwa kwa kutumia vyombo vya dola.

Ujumbe unaendelea kushutumu kuwa vyombo vya habari vimefungiwa au kusimamishwa kwa muda, uhuru wa Mahakama na Bunge unaminywa na kwamba katika mazingira haya ni rahisi kwa jamii kufarakana na hata kujenga chuki kiasi cha kuhatarisha amani, usalama na hadhi ya uhai wa binadamu.

Ujumbe umeongeza shutuma nyingine kuwa chaguzi zinaharibiwa kwa vurugu na hivyo kuacha nyuma uchungu, hasira, tamaa ya kulipa kisasi na hata kususia chaguzi nyingine na kwamba hali hiyo ni hatari kwa mustakabali wa Taifa letu, ikiachwa izoeleke tusishangae huko mbele kujikuta katika mifarakano mikubwa zaidi itakayobomoa misingi ya amani na umoja wa kitaifa.
NIMEPATA TAARIFA ZA UHAKIKA KABISA kuwa ujumbe huu haukuandikwa na Maaskofu 35 wa Kanisa Katoliki kama ilivyotolewa na Baraza la Maaskofu (TEC).

Katika shauku yangu hii ya kutaka kujua kwa nini viongozi wangu wa Kanisa lenye heshima hapa nchini wamefikia hatua hii nimepata taarifa za uhakika kuwa Maaskofu walioshiriki kuandika ujumbe huu ni wanne (nitawataja huko mbele) na Maaskofu wengine walikataa kushiriki kikao kilichofanya kazi ya kuandika ujumbe huu.

Mniwie radhi sana nimepata mashaka makubwa sana niliposoma majina ya Maaskofu waliofanya kazi ya kuandika ujumbe huu na historia zao za mahubiri yenye uchochezi mkubwa na hata mara kadhaa wametuhumiwa kwa ukabila na uchochezi na ushahidi upo.
Maaskofu walioandika ujumbe huu ni Mhashamu Askofu Mkuu Beatus Kinyaiya wa Jimbo Kuu la Dodoma, Mhashamu Askofu Mkuu Yuda Thaddaeus Ruwa’ichi wa Jimbo Kuu la Mwanza, Mhashamu Askofu Augustino Shao wa Jimbo la Zanzibar na Mhashamu Askofu Severine Niwemugizi wa Jimbo la Rulenge-Ngara.

Maaskofu wengine hawakushiriki kuandika ujumbe huu na kwa kuwa wanatambua dosari iliyokuwa inafanyika wakatoa udhuru mbalimbali na kwa hivyo hao Maaskofu wanne wakaifanya kazi hiyo wakishirikiana na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Padre Raymond Saba na wakamchukua Dk. Kasala kama mshauri wa uandishi wa ujumbe huo.

Kwa kuangalia safu hiyo utaona ujumbe huu umeandikwa pasi kuwepo Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania Mhashamu Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa wala Mwadhama Polyacarp Kardinali Pengo wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam.
Nimepata taarifa kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Songea Mhashamu Damian Dallu aliondoka mkutanoni na kuomba udhuru baada ya kubaini mwelekeo wa ujumbe huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...